• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Waziri Jaffo asisitiza agenda ya kutaka Mabadiliko Meatu.

Imewekwa: October 22nd, 2018

Na Linus R. James - MEATU DC

Mh Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI , Mh. Suleiman Said Jaffo amesisitiza agenda ya kuleta mabadiliko kwa wananchi wa Meatu mapema leo akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu.

“Wananchi walimchagua Mh. Dk. Magufuli kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuleta mabadiliko” Alisisitiza Jaffo.

Alisema kuwa ili kuleta mabadiliko katika sekta ya utumishi wa umma watumishi wanatakiwa kuondoa uzembe kazini na kushugulikia kero za wananchi.

“Fedha zinaweza kuja lakini zikikosa usimamizi hazitakuwa na maana na sisi watumishi ndio tumepewa dhamana ya kusimamia, sitaki watendaji wazembe katika ofisi yangu” alisisitiza.

Aliongeza pia kwa kutaja idara mbali mbali na kujaribu kuzikumbusha umuhimu wake katika kuleta mabadiliko kwa wananchi  huku akikisisitiza suala la mipango mizuri ya Halmashauri, ukusanyaji mapato na tathimini ya utendaji kazi wa watumishi (OPRAS) huku akisisitiza Wahandisi wasimamie miradi vizuri na zabuni wapewe wakandarasi wenye uwezo.

Aidha Mh. Waziri amefafanua suala la kuipa halmashauri ya wilaya ya Meatu kipaumbele hasa kwenye  sekta ya afya kwa kujitahidi kuwaletea miradi mingine ya vituo vya afya pamoja na kuongeza watumishi wengine.

Mapema akisoma taarifa ya mandeleo ya Wilaya ya Meatu, Mkurugenzi mtendaji Ndg. Fabian Manoza alibainisha changamoto mbali mbali zinazoikumba wilaya ya Meatu ikiwa ni pamoja na upungufu wa watumishi, madeni kwa watumishi, wakandarasi kutokuwa na uwezo katika miradi, pamoja na upungufu wa miundo mbinu ya afya.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dk. Joseph Chilongani wakati akimkaribisha waziri alimwambia kuwa watumishi wana hamu kubwa ya kumuona hivyo anamshukuru sana kwa kupata nafasi ya kutembelea wilaya ya Meatu.

Ziara ya Mh. Jaffo ilianza kwa kutembelea mradi wa hospitali ya Wilaya ya Meatu huku akiambatana na viongozi mbali mbali amabao ni Mbunge wa Jimbo la Meatu M.  Salum Khamis Salum, Mbunge Viti maalum, Mh. Leah Komanya , Viongozi wa CCM Mkoa na Wilaya pamoja na Viongozi wa mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Meatu.

Mh Jaffo amehitimisha ziara wilayani Meatu kwa kusisitiza “Ndugu zangu, Ukitaka kuruka, agana na nyonga”.  Huku akisisitiza kuwa mapungufu yote yaliyopo ndani ya Wilaya yatatuliwe haraka ili wilaya iendane na suala la mabadiliko.

MWISHO


Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.