• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

TAKUKURU RAFIKI

Imewekwa: January 27th, 2023

Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Meatu, Tibalilila Fabianus amewasilisha programu iitwayo TAKUKURU RAFIKI ambayo imebuniwa na kuzinduliwa na Taasisi hiyo hivi karibuni kwa lengo la kuwafikia wananchi katika maeneo yao na kusikiliza changamoto zinazowakabili.

Fabianus ameyasema hayo alipokaribishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu muda mfupi baada ya kufungua kikao maalum cha Baraza la Madiwani ambacho kimefanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu tarehe 27 Januari 2023 kujadili taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2021/2022, nusu mwaka wa fedha 2022/2023 na mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024.

"Tunafikiri changamoto zinazowakabili wananchi zisipotatuliwa zinaweza kusababisha vitendo vya rushwa hivyo kupitia programu hii tutaweka mikakati ya pamoja ya kutafuta ufumbuzi wa kuzitatua." Anasema Fabianus na kuongeza;

"Utekelezaji wa programu ya TAKUKURU RAFIKI utafanyika katika ngazibya kata kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kama vile Kamati za Maendeleo ya Kata- WDC's, Viongozi wa Dini na Wawakilishi wa Wananchi."

Fabianus amesema vitafanyika vikao ngazi kata ambapo Diwani wa Kata husika atakuwa Mwenyekiti, Mtendaji wa Kata atakuwa Katibu, Maafisa wa TAKUKURU watakuwa waratibu wa vikao hivyo na wadau wengine watakuwa Wajumbe.

Kaimu Mkuu huyo wa TAKUKURU amesema programu hiyo inatarajiwa kuanza utekelezaji wake mwezi Februari 2023 na ameomba ushirikiano wa viongozi hao katika maeneo yao.

Aidha, Baraza la Madiwani limeridhia na kupitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo imekadiria kukusanya na kutumia shilingi bilioni 39.97. 

Kati ya fedha hizi Mapato ya Ndani ni shilingi bilioni 3.22 na kufanya ongezeko la asilimia 10 ukilinganisha na Bajeti ya mwaka 2022/2023 ambapo Bajeti ya Halmashauri ilikuwa shilingi bilioni 38.3.

Matangazo

  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Mwaka 2023 December 14, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba (PSLE) 2022 December 01, 2022
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani November 30, 2022
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Zoezi la Kitaifa la Chanjo ya Polio Awamu ya Nne November 30, 2022
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.