• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Meatu Pikipiki Tisa

Imewekwa: February 14th, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango amewaagiza Watendaji wa Kata na Viongozi wa Mikoa wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini - TARURA kutumia ipasavyo magari na pikipiki zilizonunuliwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) katika kuwafikia wananchi kwa urahisi, kuwasikiliza, kuwahudumia, kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na siyo kutumia kwa manufaa binafsi.

Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa hafla ya kukabidhi magari 54 kwa TARURA pamoja na Pikipiki 916 kwa Watendaji Kata nchini katika hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Halmshauri ya Jiji la Dodoma, Mtumba tarehe 14 Februari 2023.

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu katika mgao huo imepatiwa Pikipiki 9 ambazo zitagawiwa kwa Watendaji wa Kata wilayani humo.

Dkt. Mpango amewaagiza Watendaji hao kutambua na kushughulikia changamoto za wananchi kwa kuhakikisha vikao na wananchi katika ngazi ya Vijiji na Mitaa vinafanyika kwa mujibu wa Sheria.

Aidha, Makamu wa Rais amewaasa Watendaji wa Kata nchini kuacha mara moja uzembe wa kusimamia miradi ya maendeleo. Amesema utoaji wa vitendea kazi hivyo unalenga kuongeza ufanisi katika ufuatiliaji wa miradi pamoja na kufuatilia Uhifadhi wa mazingira kwa kutoa hamasa kwa Wananchi kupanda miti na kuimarisha shughuli za usafi wa mazingira ili kuwepo na maendeleo endelevu.

Dkt. Mpango amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuimarisha mfumo na utendaji wa Serikali za Mitaa, kwa kuzingatia misingi ya Kikatiba na Kisheria iliyopo kwani Serikali za Mitaa ndiyo njia pekee ya kusogeza huduma kwa Wananchi kwa kuwa unawashirikisha Wananchi katika kuamua, kupanga na kuchagua vipaumbele vya maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.


Matukio katika Picha:

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango akimkabidhi pikipiki Afisa Mtendaji wa Kata ya Ng’ong’ona (wa pili kulia) iliyopo mkoani Dodoma kwa niaba ya Watendaji wengine wa Kata nchini ambao wamepata mgao wa Pikipiki 916. Pikipiki hizo zimenunuliwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) na kutolewa kwa Watendaji wa Kata nchini katika hafla iliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mtumba tarehe 14 Februari 2023. Wa kwanza kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki (Mb). (Picha zote na Ofisi ya Makamu wa Rais).



Matangazo

  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Mwaka 2023 December 14, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba (PSLE) 2022 December 01, 2022
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani November 30, 2022
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Zoezi la Kitaifa la Chanjo ya Polio Awamu ya Nne November 30, 2022
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.