• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Watakiwa Kuzuia Ulemavu Usio wa Lazima

Imewekwa: September 1st, 2022

Na Benton Nollo, Mwanhuzi

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Fauzia Ngatumbura ametoa wito kwa wazazi na walezi wilayani humo kuzuia ulemavu usio wa lazima kwa kuwapeleka watoto wenye umri chini ya miaka 5 kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili wapatiwe Chanjo ya Kuzuia Ugonjwa wa Kupooza (Polio).

Ngatumbura ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Utoaji wa Chanjo Dhidi ya Ugonjwa wa Polio mzunguko wa tatu, uliofanyika katika Hospitali ya WIlaya ya Meatu mapema leo tarehe 01 Septemba 2022.

“Tunaweza tukaua uchumi wa nchi au nguvu kazi kwa namna nyingi, hata wewe mama ambaye umezaa mtoto wako vizuri halafu ikatokea hujampa chanjo ya polio akapata ulemavu familia hiyo inaweza ikajikuta inaingia kwenye umaskini mkubwa kwa sababu muda mwingi utakuwa ni wa kumhudumia mtoto.” Anasema Ngatumbura na kuongeza;

“Tumeona maeneo mengine mama kazi yake haendi kulima haendi kufanya biashara, kazi yake ni kukaa na mtoto mlemavu ambaye ulemavu wake umesababishwa na ugonjwa wa Polio, wewe utakuwa kazi yako ni kumhudumia muda wote…wananchi tuzuie ulemavu wa watoto usio wa lazima, hatukatai yawezekana Mwenyezi Mungu anampa mtu ulemavu wa aina nyingine, lakini usiwe ni ulemavu unaotokana na kwamba mtoto wa Kitanzania kukosa Chanjo ya Polio.”

Ngatumbura amewahimiza Wananchi kuisemea chanjo hiyo inayotolewa kwa njia yam atone, maeneo yote ili wananchi wote wapeleke watoto wao kupata chanjo hiyo muhimu kwa watoto na amewahakikishia kuwa chanjo hiyo ni salama na ni kwa maslahi ya watoto wa Kitanzania.

Aidha, Ngatumbura amewahimiza wananchi wote kuwa mabalozi ili zoezi hilo liweze kufanikiwa katika malengo yaliyokusudiwa kwani taifa linalengo la kuwaweka watu wake salama baada ya kuwepo kwa dalili za ugonjwa huo katika nchi jirani.  

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Msoleni Dakawa ametumia fursa hiyo kumpongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi hasa katika suala zima la kulinda na kuboresha afya za wananchi anaowaongoza kwa kuwekeza fedha nyingi katika sekta hiyo muhimu nchini.

“Sisi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu tupo tayari kuhakikisha zoezi hili linafanikishwa kwa zaidi ya asilimia 100, kwa sasabu tumeshajipanga vizuri…niwaombe sana viongozi wenzetu ambao wapo kwenye ngazi ya wananchi…tushirikiane kwa pamoja tuhamasishe wananchi wapeleke watoto wao kwenye vituo vya kutolea huduma vili waweze kupata chanjo hiyo ambayo ni muhimu sana.” Amesema Dakawa.

Awali, akitoa taarifa ya uzinduzi wa Kampeni hiyo kitaifa, Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Wilaya ya Meatu, Dkt. Frank Mganga amesema katika mzunguko wa pili Halmashauri hiyo ilipokea dozi 132,600 kwa lengo la kuwafikia watoto chini ya miaka 5, 115,301 katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya 53, vituo visaidizi 85 na huduma tembezi za nyumba kwa nyumba ambapo Halmashauri ilifanikiwa kuchanja watoto 139,953 sawa na asilimia 121.

Dkt. Mganga amebainisha kuwa katika mzunguko wa tatu ulioanza leo tarehe 01 hadi 04 Septemba 2022, Halmashauri imepokea chanjo 149,000 kwa lengo la kuchanja watoto 144,140, vibebea chanjo 216, mabango na vipeperushi 100 pamoja Reflector 100.

Kauli Mbiu ya Kampeni ya Chanjo ya Polio ni; Mpe Chanjo, Okoa Maisha ambayo inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na wafadhili wa Shirika la Umoja wa Taifa Linalohudumia Watoto - UNICEF pamoja na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) ambapo lengo likiwa kuokoa maisha ya watoto.


Matukio Katika Picha Wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Utoaji wa Chanjo Dhidi ya Ugonjwa wa Polio Mzunguko wa Tatu ambayo Inafanyika kwa siku Nne (tarehe 01 hadi 04 Septemba 2022)


Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.