• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Watakahojihusisha na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi Meatu kukiona

Imewekwa: February 25th, 2019

Na Linus R James - MEATU DC

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu Ndg. Fabian Manoza mapema leo alipofanya ziara katika shule ya Sekondari Mwanjoro na  kuzungumza na wazazi, walimiu, wanafunzi na watumishi wa kata ya Mwanjoro.

Katika kikao hicho kilichokua na lengo la kupanga mkakati wa namna ya kupata utatuzi wa changamoto ya upungufu wa viti na meza(madawati) kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari Mwanjoro mkurugenz huyo licha ya kuahidi kutoa mifuko 100 ya saruji, madawati 10 pamoja na kutoa motisha kwa mwanafunzi yoyote atakayepata daraja la kwanza(div one) pia ameguswa sana na kupongeza  jitihada mbali mbali zinazofanywa na uongozi wa kata hiyo kwa kushirikiana na uongozi wa halmashauri pamoja na wanakijiji katika kuinua elimu ikiwa ni pamoja najitihada za kujenga bweni la wanafunzi wa kike ambalo lipohatua ya lenta ya pili na ujenzi unaendelea.

Akizungumza na wanafunzi na walimu baada ya kikao cha wazazi Mkurugenzi huyo ametoa ahadi ya shilingi elfu hamsini kwa mwanafunzi yeyote atakayetoa taarifa kwa mtu yeyote atakayejihusisha kimapenzi na mwanafunzi.

Licha ya kutoa ahadi hiyo Mkurugenzi huyo ameoneshwa kukerwa na na matokeo yasiyoridhishwa  ivyo kuhahidi kumshughulikia mtu yeyote atakayejihusisha kimapenzi ikiwa ni pamoja na wanafunzi, walimu au wanakijiji.

"Lakini huku bado tuko nyuma, matokeo ya kidato cha nne kwa miaka mitatu mfululizo bado hatufanyi vizuri hata kimkoa, mwaka huu kidogo tumeinuka, nawashukuru sana walimu na wazazi ambao sasa wameinuka na viongozi wetu kwa ushirikiano tunaoupata, lakini kiukweli bado tunahitaji jitihada za ukweli kuhakikisha wanafunzi wetu wanafanya vizuri" Alisema Ndg. Manoza

Katika kikao hicho chenye lengo la kupata madarasa, wanakijiji wa Kata ya Mwanjoro na Mbushi wameahidi kutengeneza madawati yanayopungua na kuyakamirisha ifikapo tarehe 25 mwezi wa tatu mwaka huu.

Akiwasalimia wazazi Mkurugenzi huyo alitaja jitihada zinazofanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania chini ya Dk. John Pombe Magufuri katika elimu na kuwaonesha ni nama gani wazazi hao wanatakiwa waoneshe kumpongeza kwa vitendo alijaribu kutoa mfano wa fedha za elimu bure zinazokuja katika shule hiyo.

"Nilikua natoa mfano wa Rais wetu wa awamu ya tano, Mh Dk John Pombe Magufuli, hela inayotoka serikalini kuja hapa mwezi mmoja tu tumepokea shilingi 531,453 mwezi mmoja tu, sasa hii ukizidisha mara kumi na mbili, ukazidisha kwa shule zote Tanzania, ni Matrilioni ya hela  Mh Rais anatoa kuwafidia watoto wetu wasome, sasa tunahitaji na sisi kumpongeza Mh Rais wetu kwa vitendo kwa yale ambayo yapo chini yetu sisi wazazi tuyafanye".

Katika kikao hicho wanakijiji hao waliweza kumchagua Ndg Ibrahim kuwa mwenyekiti, wazazi wawili(mmoja kutoka kila kata) kuwa makatibu wa kusimamia zoezi hilo  amabapo zoezi hilo kila dawati litakua na thamani ya shilingi elfu 40 ambapo fedha zitakusanywa na madawati yatatengenezewa mjini Mwanhuzi. Aidha Mkurugenzi huyo ameahidi ofisi yake kutoa gari ambalo litayasafirisha madawati hayo pindi yatakapokamilika kutoka Mjini Mwanhuzi mpaka shule ya Sekondari Mwanjoro.

Pia mkurugenzi ametoa ahadi ya ofisi ya Mkurugenzi mtendaji kumsomesha kuanzia kidato cha tano hadi cha sita popote pale atakapochaguliwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mwanjoro  aliyefanya vizuri kimasomo katika matokeo ya kidato cha nne ambapo amepata daraja la kwanza

Kikao hicho kiliudhuriwa na wakuu wa idara mbali mbali za Halmashauri ya Wilaya ya Meatu,Mh  Diwani wa viti maalumu pamoja na Mh  Diwani wa kata ya mwanjoro na wataalamu mbali mbali ngazi ya Kata ya Mwanjoro na Mbushi.

Mwisho.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.