• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Wafugaji wasisitizwa kuzingatia taratibu, sheria na miongozo ya nchi ili kufikia ufugaji wenye tija

Imewekwa: April 21st, 2019

Na Linus R. James (MEATU DC)

Hayo yamesisitizwa jana na katibu mkuu wa Mifugo katika Wizara ya maendeleo ya mifugo na uvuvi Prof. Ole Sante Ole Gabriel  katika kikao kazi chake kati ya uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Meatu pamoja na wafugaji wa Wilaya ya Meatu.

“Tunatamani fikra za wafugaji wa Meatu na kote nchini, zibadilike na ziweze kutambua umuhimu wa sheria, taratibu na kanuni, Niwaombe wafugaji wa Meatu, simiyu, kanda ya ziwa na  Tanzania nzima popote walipo watambue kwamba Wizara ya mifugo ya uvuvi itapenda wafugaji wake wafuate kanuni, taratibu na miongozo” Alisema Ptof Ole Sante

Licha ya kusisitiza umuhimu wa kufuata sharia za nchi  Katibu mkuu huyo alisisitiza mambo makuu manne aliyokuja kuyasisitiza kubwa likiwa ni umuhimu wa kufata sharia na taratibu za nchi, mengine yalikua ni masuala ya uhamirishaji, Ufugaji wa kisasa uunganike na uchumi wa viwanda

Pamoja na Wakulima wkutobweteka na mifugo wajali uchumi wao ikiwa ni  kuvaa vizuri na kuwa na maisha mazuri.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu Ndg. Fabian Manoza  mbali na kutoa shukrani alibahinisha jitihada na mikakati ambayo Halmashauri ya wilaya ya Meatu inafanya ili kuboresha kiwanda cha maziwa ambapo tayari kupitia Wizara ya Kilimo tayari mashamba darasa ya malisho yamepandwa katika shamba la Halmashauri ya Wilaya ya Meatu na katika kata ya Lubiga ikiwa ni jitihada za kuwa na uhakikika wa malisho.

Pia alikielezea kikao kuwa tayari halmashauri ya Wilaya imeanza kugawa mbegu za uhamirishaji na baadhi ya wafugaji walipo katika kikao tayari wameshaanza kutekeleza suala la uhamirishaji.

Viongozi mbali mbali wa Wilaya akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dr. Joseph Chilongani, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (W) Meatu Ndg. Juma Mwiburi waliweza kumshukuru Katibu mkuu kwani safari yake imeonesha na kuboresha hali ya mawasiliano na ukaribu baina ya uongozi wa Wilaya ya Meatu na wafugaji ambao ni wananchi wanaowatumikia.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi mbele ya kikao diwani wa kata ya Mwasengera Mh Saakumi aliwasisitiza wafugaji wenzake suala la kuzingatia taratibu na sheria ziheshimiwe

“Tatizo tulilokua tunaliona ni kati ya wahifadhi wanaotekeleza sharia na sisi, Upo ubabe uliokuwa unazidi sana, vitu ambao tumebaini kwenye kikao chetu ni sisi viongozi na wahifadhi, tatizo tulilo nalo sisi ni pale tunapokamatwa, katika kikao chetu cha ndani tumefikia muafaka kuwa sisi ni wamoja kati ya wahifadhi na viongozi” Alisema Mh Saakumi

Katika kikao hicho Mwenyekiti wa CCM wilaya alipewa jukumu la kukutana na wafugaji kwenye maeneo yao ya ufugaji ndani ya wiki mbili kuhakikisha changamoto na kero zote zinajadiliwa na kutatuliwa haraka ili Wilaya ya Meatu iwe na ufugaji wenye tija.

MWISHO

Picha zaidi Bofya Hapa

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.