• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Taasisi zote za umma , Meatu zahimizwa kufanya kazi kwa weledi

Imewekwa: June 24th, 2021

Anaandika Linus R. James

Hayo yamesemwa na  Mkuu wa Wilaya ya Meatu Bi Fauzia Hamidu Ngatumbura  katika hafla fupi ya kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Meatu Dr. Joseph E. Chilongani.

“Nianze na taasisi za umma zote zilizopo ndani ya Meatu, wote tunatekeleza Ilani ya chama cha Mapinduzi basi tutumie uwezo wetu wote kutekeleza kila mtu kwa wakati wake, kwa nafasi yake, kwa uwezo wake ambao Mungu amemtunuku na kwa ushirikiano mkubwa, ni vema tukapeana taarifa mara kwa mara kwa sababu mapungufu tunayo ili tuweze kurekebishana huku tukiendelea na safari”. Alisema Mh. Ngatumbura wakati akiwasalimu wananchi baada ya ukaribisho

Mh Ngatumbura amevihimiza pia vyama vya wafanyakazi wawaelimishe watumishi (wanachama wao) kwa kuwaelimisha kuhusu miongozo na taratibu za utumishi wa umma ili kusudi watumishi wafurahie utumishi wao na hatimaye utendaji kazi wa watumishi uboreke zaidi.

Naye Mkurugenzi wa Wilaya  ya Meatu Bw. Fabian Manoza Said akitoa salaam na kutambulisha watendaji wa halmashauri kutoka makao makuu mpaka ngazi ya vijiji aliyataja mafanikio ambayo yamefikiwa katika uongozi wa Dr. Chilongani ikiwa ni pamoja na kupanda kwa kiwango cha ufaulu wa elimu kuanzia msingi mpaka  sekondari pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa kilimo cha zao la pamba katika wilaya ya Meatu.

Hata ivyo Mkurugenzi huyo wa wilaya ya Meatu amesisitiza kuwa vipaumbele vilivyopo katika wilaya ya Meatu ni kuhakikisha wilaya, inaboresha miundombinu hususani, elimu na vituo vya kutolea huduma za  afya.

“Kwenye mapambano haya mda mwingine unakuta mnasuguana, lakini mnasuguana kwa mazuri, kwenye elimu kidato cha nne kuanzia 2016 tulikua tunapandisha ufaulu kuanzia asilimia 69, mwaka unaofuata 78%, mwaka unaofuata72%, mwaka unaofuata87%, na matokeo yaliyopita asilimia 92”. Alisema Manoza ambapo alisisitiza kuwa ufaulu pia umekua ukipanda sana pia katika upande wa elimu msingi.

Kwa upande wa wananchi, Manoza amesema kipaumbele cha wilaya ni kuhakikisha uzalishaji wa zao la pamba unaongezeka kwa ekari kutoka kilo 200 kwenda mpaka kilo 600.

Naye aliyekuwa mkuu wa wilaya Dr. Chilongani akitoa salam na kuwaaaga wananchi pamoja watumishi waliodhuria hafla hiyo hakusita kuyataja mafanikio yaliyofikiwa na kumtakia kila lakheri Mkuu wa Wiaya ya Meatu.

“Mengi yameelezwa na  mkurugenzi akifafanua mafanikio ambayo tumeyapata pamoja kama timu ya wana Meatu, kwa kweli tumejitahidi sana hasa kwa upande wa elimu, timu nzima ya wana Meatu tuliweza kuhakikisha tunalifanya vizuri na nina Imani zile asilimia zilizobaki  kufikia asilimia 100 mtazitekeleza chini ya usimamizi wa Mh . Fauzia” Alisema Dr . Chilongani.

Hafla hii ya Kumuaga Chilongani na Kumkaribisha Bi Ngatumbura imefanyika katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Meatu ambapo makabidhiano ya ofisi pamoja na taasisi zilizoko ndani ya wilaya ya Meatu yamefanyika na kisha kufuatiwa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Meatu ambapo watumishi mbalimbali kutoka idara za afya, utumishi na afya wamepewa zawadi pamoja na kutunukiwa vyeti kutokana na utendaji kazi.

Bi. Faudhia Hamadi Ngatumbula anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Meatu wa kumi na moja (11) toka wilaya  ianzishwe baada ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Meatu na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan Tarehe 19 Juni 2021.

MWISHO


Picha zaidi za matukio bofya hapa

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.