• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Taarifa ya rufaa ya vyeti feki kwa Watumishi wa Umma kutolewa tarehe 30 Juni, 2017

Imewekwa: June 25th, 2017

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurian Ndumbaro amesema taarifa ya rufaa ya watumishi waliobainika kuwa na vyeti feki itatolewa Juni 30, mwaka huu, 2017.

Dkt Ndumbaro ameyasema hayo wakati alipozungumza na viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya, ambao ni wasimamizi wa Watumishi wa Umma Mkoani Simiyu katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi nchini.

Amesema katika zoezi la uhakiki la awamu ya kwanza Watumishi zaidi ya 9,000 walibainika kuwa na vyeti feki ambapo kati yao ni asilimia kumi tu (10%) ndiyo waliokata rufaa.

“ Taarifa itawasilishwa tarehe 30 mwezi huu na baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya rufaa hizo  maelekezo yatatolewa namna ya kuhitimisha ajira za watu wenye vyeti feki” amesema

Aidha, amesema baada ya taarifa ya rufaa kuwasilishwa Serikali itatangaza vibali vya nafasi za ajira kwa watumishi watakaojaza nafasi zitakazoachwa wazi na zile zilizotengwa.

Wakati huo huo Katibu Mkuu huyo amewataka viongozi wasisite kuwachukulia hatua watumishi wanaokiuka sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma na kuwapongeza wanaofanya kazi kwa bidii ili kuwapa motisha.

“Kusiwe na masuala ya kuhamisha watumishi wanaosumbua, kama mtu anasumbua malizana naye pale pale fuata taratibu mfungulie mashtaka,  ili tujenge utumishi wa Umma wenye uadilifu na weledi, lakini pia wale wanaofanya kazi vizuri wapongezeni mkiwaacha mtawakatisha tamaa” alisema.

Kuhusu suala la Watumishi kupandishwa vyeo Dkt.Ndumbaro amesema lifanyike kama motisha kwa watumishi wanaofanya kazi vizuri kwa kuzingatia ufanisi katika utendaji wa kazi,bajeti, masharti mengine ya upandaji vyeo kwa watumishi likiwepo la kufanya kazi kwa muda usiopungua miaka mitatu katika cheo kimoja.

Katika hatua nyingine Dkt. Ndumbaro amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuwasimamia Maafisa Utumishi wanaosimamia mfumo wa mshahara wa LAWSON kuhakikisha wanaunganisha taarifa za mfumo huo na takwimu za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA kwa ufasaha na kuwakumbusha watumishi kuangalia taarifa zao ili wazihakiki ikiwa ziko sahihi na halali.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Watumishi wa Umma mkoani Simiyu, Katibu Tawala Mkoa ameahidi kutekeleza na  kuhakikisha watendaji wengine wanatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Katibu Mkuu ili Utumishi wa Umma ufanyike katika maadili, ufanisi na weledi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Ndg.Mariano Mwanyigu ameshauri Serikali iangalie kwa upya umri wa kustaafu kwa hiari ambao ni miaka 55, kwa mujibu wa sheria miaka 60 na kuona uwezekano wa kupunguza miaka ili kutoa nafasi kwa vijana wengi walio nje ya mfumo kupata ajira.

Kikao hicho ambacho pia kimetumika kutoa taarifa, maagizo na maelekezo mbalimbali kimewashirikisha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Sekretarieti ya Mkoa, Makatibu Tawala wa Wilaya,Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri na Maafisa Utumishi wanaoshughulikia Mfumo wa mshahara wa  LAWSON.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.