• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Simiyu yazindua upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kwa kutumia teknolojia ya ndege nyuki ("Drones")

Imewekwa: September 19th, 2018

Mkoa wa Simiyu umezindua Mpango wa kupima maeneo ya wafugaji na wakulima kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya ndege nyuki (drones) lengo likiwa ni kuwawezesha kuyatambua maeneo yao na kupewa hati miliki na baadaye kuyawekea miundombinu muhimu ya ufugaji na kilimo na kuondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Zoezi hilo limezinduliwa na  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka katika kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu na linatekelezwa Chini ya Serikali kwa Kushirikiana na Taasisi Ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ESRF).

Amesema Mkoa huo ndiyo unaoongoza kwa kilimocha pamba nchini na ni miongoni mwa mikoa yenye ng’ombe wengi nchini, kwa kuwa wakulima na wafugaji wanamiliki ardhi ni vema maeneo yao yakapimwa wakapewa hati miliki na baadaye watalaam wa ardhi wawasaidie kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Ameongeza kuwa wafugaji wa mkoa wa Simiyu wamekuwa wakitozwa faini katika maeneo mbalimbali hivyo ili kuondokana na kadhia hiyo maeneo yao yakipimwa na wakaweka miundombinu muhimu kama vile mabwawa, visima, majosho na maeneo ya malisho wataondokana na uchungaji wa mifugo na kwenda kwenye ufugaji wenye tija

“Tungehitaji mpime mashamba yenu yakishapimwa mtapewa hati, watalaam wa halmashauri watawatengenezea mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuwashauri namna sahihi ya uwekeaji wa miundombinu kama majosho, mabwawa, visima ili muwe wafugaji wenye tija ambao hamtapigwa faini wala kuibiwa ng’ombe” alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Mfumo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Bw. John Kajiba amesema upimaji kwa kutumia teknolojia ya ndege nyuki utafanyika  kwa urahisi  na haraka zaidi na ikilinganishwa na upimaji wa watu moja kwa kwa moja.

“Uzuri wa kutumia ndege nyuki ni kwamba tutatumia muda mfupi sana kupima eneo kubwa kwa wakati mmoja mfano,  eneo ambalo lngeweza kupimwa na watu wane kwa muda wa siku nne drone(ndege nyuki) inafanya kwa muda wa siku moja” alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa amesema upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji utawasaidia kutatua migogoro kati ya wakulima na wafugaji na kupata hati ziatazowasaidia kuchukua mikopo kwenye taasisi za kifedha na kufanya shughuli za maendeleo kupitia maeneo yao

Nao wananchi wa Meatu wanasema wameupokea mpango huo kwa mikono miwili  kwa sababu watakuwa na uhakika wa umiliki wa maeneo yao baaada ya kupewa hati ambazo pia wamesema zitawasaidia kukopa mitaji ya kufuga na kulima kisasa na kwa tija.

“ Tumeupokea mradi huu kwa mikono miwili maana tutakapopimiwa maeneo yetu tutakuwa tunakopesheka kwenye taasisi za fedha, vile vile tutakuwa tumeondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji kwa sababu maeneo yetu yatakuwa na mipaka iliyo wazi na kila mmoja atakuwa na hati ya kumili eneo lake” alisema John Mchagula mfugaji kutoka Kijiji cha Ng’hoboko

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.