• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Ombi la wananchi wanaopakana nahifadhi ya pori Maswa kufikishwa kwa Rais JPM

Imewekwa: February 19th, 2019

Mwenyekiti wa Timu maalum ya mawaziri wanane ya kupitia maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na maeneo ya Hifadhi ambaye ni Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo na Makazi Mhe. Wiliam Lukuvi amepokea ombi la wananchi wa wilaya tatu za mkoa wa Simiyu wanaoishi katika vijiji vinavyopakana na Pori la akiba la Maswa la kupewa eneo lenye urefu wa kilometa kumi, kwa ajili ya malisho na kuahidi kulifikisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua zaidi.

Mhe. Lukuvi ameyasema hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vinavyopakana na pori la akiba la Maswa katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mji mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu.

Awali akijibu baadhi ya kero zilizowasilishwa na Mwananchi wa Wilaya ya Meatu, Bw. Deusdedith Martin Waziri Lukuvi amesema timu hiyo imezisikia kero hizo na akaahidi kuwasilisha taarifa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na kubainisha kuwa taarifa rasmi ya majibu ya kero zao itatolewa.

Aidha, Waziri Lukuvi amewahakikishia wananchi kuwa zoezi la kupima eneo la mita 500 kutoka kwenye mpaka wa Pori la Akiba la Maswa kuelekea kwenye vijiji vinavyopakana na Pori hilo (Buffer zone) katika Wilaya za Meatu, Itilima na Maswa limesimamishwa mpaka litakapotolewa maelekezo.

“Hapa kulikuwa na zoezi la kupima mita 500 kutoka kwenye mpaka wa Pori la Akiba la Maswa kuingia kwa wananchi, maana yake ni kwamba kuna wananchi wengi na vijiji vingi vingeathirika ili vipishe ‘buffer zone’, ingawa ni kwa mujibu wa sheria lakini ‘buffer zone’ ile ingekula maeneo ya vijiji kwa hiyo zoezi hilo limesimamishwa”

“Zoezi hili limesimamishwa kwa mujibu wa maelekezo ya Mhe Rais baada ya kuona watu wengi maskini ambao walipaswa kupisha maeneo ya hifadhi;...... vile vile kuanzia sasa zoezi lolote la kutambua mipaka litakalofanywa na watu wa Maliasili ni lazima liwe shirikishi” alisema Waziri Lukuvi.

Awali akiwasilisha taarifa kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Meatu, Bw. Deusdedit Martin aliomba Timu ya Mawaziri wanane kuwasaidia katika kutatua changamoto ya ubadilishaji wa mpaka kati ya Pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyopakana, Uvamizi wa tembo katika mashamba na makazi ya watu na kukatazwa kwa wananchi kulima katika eneo la mita 60 kutoka kwenye kingo za mito.

Kwa upande wake Waziri wa Maji, Mhe. Prof. Makame Mbarawa amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Simiyu upatikanaji wa uhakika wa maji kupitia mradi mkubwa wa Ziwa Victoria, ambapo amesema kwa sasa mradi upo katika hatua ya kumtafuta mkandarasi

Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe.Omari Mgumba akieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inatoa viatiifu kwa wakulima ambapo amesema hadi sasa zaidi ya chupa milioni saba zimeshasambazwa kwa wakulima katika mikoa inayolima pamba hapa nchini.

Timu ya Mawaziri wanane inayoongozwa na Waziri Lukuvi pia inajumuisha mawaziri kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Maliasili na Utalii, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Maji na Manaibu Waziri kutoka Wizara ya Kilimo na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira.

Mwisho

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.