• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa aongoza viongozi na wananchi Simiyu Mazishi ya Mh Mahega

Imewekwa: June 14th, 2018

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa, Dkt. Edmund B. Mndolwa aliwaongoza viongozi wa CCM Taifa na Mkoa wa Simiyu na Shinyanga, pamoja na  viongozi wa Serikali Mkoa wa Simiyujana katika kijiji cha Zebeya wilayani Maswa kwenye mazishi ya aliyekua diwani wa kata ya Tindabuligi wilaya ya Meatu  marehem Seleman Mahega.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Dkt. Mndolwa ametoa pole kwa familia ya marehemu Mahega na akawaomba ndugu na familia kuwa na subira katika kipindi kigumu walichonacho.

Amesema Mhe. Rais anatoa shukrani kwa Kituo cha Afya Mwandoya, Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu, Hospitali ya Rufaa Bugando na Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa namna walivyowahudumia majeruhi 19 wa ajali hiyo ambapo baadhi yao walitibiwa na kuruhusiwa na wengine bado wanaendelea kupata matibabu.

Aidha, Dkt. Mdolwa amemshukuru Mbunge wa Kisesa ambaye pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina kwa kuchukua maamuzi ya haraka ya kukodi ndege iliyowapeleka majeruhi tisa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa ajili ya matibabu na uchunguzi zaidi.

Naye mwenyekiti wa UVCCM Mh Kheri James amabaye ndiye alikua katika msafara wakati ajali ilipotokea alipataa nafasi ya kutoa salamu zamwisho

“Ndugu yangu aliyelala mbele yetu hapa, alinipokea mimi akanishika  mkono na akaniambia mwenyekiti tumejiandaa kukupokea, Itilima hawawezi kutufunika sikujua kama Itilima walikua hawawezi kutufunika kwa staili hii, wala sikujua kwamba zile zilikua ni salamu za kuniaga na kuniambia kwamba mapokezi yale hayatakua mapokezi tena baada ya hapo” Alisema James wakati akitoa salamu za mwisho

“Nilitegemea atashirikiana na wajumbe wenzake wa halmashauri kuu ya CCM kunieleza chama kinaendeleaje kwenye wilaya yao, nlitegemea nitashirikiana naye na viongozi kuona tunafanyaje katika vikao vya serikali na chama kuona serikali nafanyaeje kufikia malengo yetu” alisistiza James  huku baadhi ya waombolezjii wakilengwa na machozi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa pole kwa familia, ndugu na Baraza la Madiwani Meatu amewashukuru viongozi wa Chama na Serikali ambao wametoa misaada mbalimbali katika kuhakikisha majeruhi wa ajali wanapata matibabu kwa wakati na marehemu anasitiriwa kwa heshima zote kama kiongozi.

Katika hatua nyingine Mtaka amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kuhakikisha kuwa stahili zote za kisheria ambazo familia ya marehemu inapaswa kupewa na Halmashauri, zitolewe mapema badala ya kusubiri kufuatwa na familia hiyo.

Naye Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa iliko kata aliyokuwa anaitumikia marehemu Mahega amewashukuru viongozi wa Chama na Serikali kwa namna walivyojitoa katika kushughulikia majeruhi na msiba ambapo pia amewashukuru wananchi wa Wilaya ya Meatu na Maswa mahali alikozikwa marehemu kwa ushirikiano na upendo mkubwa waliounesha katika msiba huo tangu siku Mhe. Mahega alipofariki mpaka kuzikwa kwake.

Mpina ametoa pole kwa familia, wananchi wa kata ya Tindabuligu na Wilaya ya Meatu kwa ujumla kwa kuondokewa na Mhe. Mahega ambaye amesema ameacha pengo kubwa kwa kuwa alikuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya wananchi na Meatu kwa ujumla.

Kwa upande wake Diwani wa Viti maalum Mhe. Avelina Kyakwambala ambaye amefanya kazi na Marehemu kama madiwani toka mwaka 2000 , amesema msiba huo umeupokea kwa masikitiko makubwa na kwamba Meatu imepoteza diwani mwadilifu, mchapakazi, anayezingatia kanuni zote za baraza, chama chake na alikuwa tayari kukosoa na kukosolewa kwa ajili ya kujenga na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Msiba wa Marehemu Mahega Selemani ambaye ameacha mke na watoto 14, umehudhuriwa na Wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Viongozi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Simiyu na Mwanza na Viongozi wa Serikali Mkoa wa Simiyu na wilaya zote mkoani humo

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.