• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Meatu Yashika Nafasi ya Pili Ukusanyaji wa Mapato

Imewekwa: August 3rd, 2022

Na Benton Nollo, Meatu

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, imeshika nafasi ya pili katika Mkoa wa Simiyu na nafasi ya 59 kwa Halmashauri zote nchini kwenye ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kigezo cha asilimia ya makusanyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Kwa mujibu wa taarifa ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serkali za Mitaa, Innocent Bashungwa (Mb) (pichani katikati) kuhusu Mapato na Matumizi ya Mapato ya Halmashauri zote 184 nchini kwa mwaka wa fedha 2021/2022 aliyoisoma jijini Dar es Salaam tarehe 02 Agosti 2022, imeainisha kwamba Halmashauri hiyo kwa kipindi cha mwaka husika ilipanga kukusanya shilingi bilioni 2.574 kupitia mapato yake ya ndani ambapo hadi kufikia mwezi Juni 2022 imefanikiwa kukusanya shilingi bilioni 2.745 sawa na asilimia 107.

Uchambuzi unaonesha kwamba, mwenendo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Juni 2022, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ni miongoni mwa Halmashauri 100 nchini zilizokusanya mapato yake kwa zaidi ya asilimia 100.

Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu imeshika nafasi ya pili katika Mkoa wa Simiyu na nafasi ya 42 katika ukusanyaji wa mapato ya ndani kwenye kundi la Halmashauri za Wilaya kuanzia Julai 2021 hadi Juni 30, 2022 kwa kigezo cha asilimia ya makusanyo.

Kwa upande wa matumizi ya mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022, Mapato yaliyokusanywa yasiyofungwa (Unprotected Revenue) katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu yalikuwa shilingi bilioni 2.324 ambapo fedha zilizopaswa kutumika kwenye miradi ya maendeleo ni shilingi milioni 929.713 ilhali fedha zilizotumika ni shilingi milioni 872.202 sawa na asilimia 38 na ambapo katika Mkoa wa Simiyu imeshika nafasi ya kwanza na nafasi ya 63 kati ya Halmashauri 184 nchini.

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu katika mikopo ya asilimia 10 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kutokana na mapato yake ya ndani iliyokusanya (shilingi bilioni 2.324) ilifanikiwa kupeleka shilingi milioni 218.064 kwa ajili ya vikundi vya Wanawake, Vijana na Wenye Ulemavu sawa na asilimia 9 ya mapato husika na hivyo kushika nafasi ya pili katika Mkoa wa Simiyu na nafasi ya 55 katika Halmashauri 184 nchini.

Kadhalika, utekelezaji wa Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2021/2022, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilikuwa na Hoja 95 ambapo zilizojibiwa na kufungwa ni 55 sawa na asilimia 57.9 ambapo katika alama 20 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilipata alama 11.6 na kushika nafasi ya pili kimkoa na nafasi ya 66 katika ya Halmashauri 184 Tanzania Bara.

Pamoja na mambo mengine, kuhusu utoaji wa mrejesho na uhabarishaji Wananchi kwa kipindi cha kuishia Mwezi Juni 2022, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilishika nafasi ya 165 katia ya Halmashauri 184.

Kuhusu Tathmini ya jumla ya Utendaji wa Haslmashauri kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2021 hadi Juni 2022, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu imepata alama 77.8 ambalo ni Dalaja B+ na kushika nafasi ya pili katika Mkoa wa Simiyu na nafasi ya 64 katika Halmashauri 184 nchini.


(Chanzo: Ni taarifa ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Innocent Bashungwa (Mb) kuhusu Mapato na Matumizi ya Mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2021/2022 aliyoisoma katika Mkutano wake na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam tarehe 02 Agosti 2022.)

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.