• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Meatu Mabingwa Nyakabindi

Imewekwa: August 8th, 2022

MEATU MABIGWA NYAKABINDI

Na Benton Nollo, Nyakabindi Bariadi

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu imeibuka mshindi kwa kushika nafasi ya Kwanza katika Kundi la Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenye Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (maarufu kama Nane Nane) Kanda ya Ziwa Mashariki mwaka 2022 ambayo yamehitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.

Akisoma taarifa ya Kamati ya Ushindanishaji na Tathmini ya Maonesho ya Nane Nane 2022, Mwenyekiti wa Kamati ya Uratibu wa Nane Nane Kanda ya Ziwa Mashariki, Beda Chamatata ameeleza kwamba Halmashauri hiyo imepata alama 95.08 na kuzishinda Halmashauri zote 21 za Mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara.

Halmashauri hizo zilishindanishwa katika maeneo matatu ambayo ni mabanda, vipando na mifugo ambapo wastani wa alama katika sehemu hizo ndiyo uliotumika kutoa mshindi wa kwanza hadi wa tatu.

Halmashauri nyingine zilizopata ushindi ni Halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Sinyanga ambayo imeshika nafasi ya pili kwa kupata alama 86.10 na Halmashauri ya Mji Bariadi mkoani Simiyu ambayo imeshika nafasi ya tatu kwa kupata alama 80.58.

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu inashika nafasi ya kwanza kwa mara ya tatu mfululizo.

Mbali na ushindi huo, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu pia imeshika nafasi ya pili katika mshindi wa jumla kwenye maonesho hayo yaliyofanyika kwenye viwanja wa Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

 Mgeni Rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ya Ajenda 10/30 Kilimo ni Biashara, Shiriki Kuhesabiwa kwa Mipango Bora ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda.

Matukio katika Picha:

Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda (wa kwanza kushoto aliyevaa Skafu) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meja Jenerali Suleiman Mzee (wa pili kushoto) kwa pamoja wakimkabidhi kombe Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya ya Meatu, Thomas Shilabu (wa kwanza kulia) baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kushika nafasi Kwanza katika Kundi la Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenye Maonesho hayo yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022 yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda (wa pili kushoto aliyevaa Skafu), Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meja Jenerali Suleiman Mzee (wa tatu kushoto) na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Festo Kiswaga (wa kwanza kushoto) kwa pamoja wakimkabidhi kombe Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya ya Meatu, Thomas Shilabu (wa kwanza kulia) baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kushika nafasi Pili katika nafasi ya mshindi wa jumla kwenye Maonesho hayo yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022 yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uratibu wa Nane Nane Kanda ya Ziwa Mashariki mwaka 2022, Beda Chamatata akisoma taarifa ya Kamati ya Ushindanishaji na Tathmini ya Maonesho ya Nane Nane 2022, wakati wa sherehe ya kuhitimisha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu tarehe 08 Agosti 2022 ambapo Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho hayo alikuwa    Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda. Maonesho hayo yalianza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Msoleni Dakawa (aliyevaa suti ya kijivu katikati) akisherehekea ushindi pamoja na baadhi ya Watumishi na Wajasiriamali walioshiriki Maadhimisho ya Wakulima Nane Nane 2022, yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu yaliyoanza tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022. Ambapo Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho hayo alikuwa    Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Fauzia Ngatumbura akipiga makofi kwa furaha baada ya Halmashauri yake kutajwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uratibu wa Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Ziwa Mashariki, Beda Chamatata (hayupo pichani) kuwa imeshika nafasi ya Kwanza katika Kundi la Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenye Maonesho hayo yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022 yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

Baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni Rasmi katika kilele cha Sikukuu ya Wakulima Nane Nane Kanda ya Ziwa Mashariki 2022, Dkt. Yahaya Nawanda (hayupo pichani)  Beda Chamatata (hayupo pichani) wakati wa kilele cha maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.

Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda (aliyevaa Skafu) akimsikiliza Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya ya Meatu, Thomas Shilabu (wa pili kulia) wakati akikagua vipando kwenye banda la kilimo la Halmashauri hiyo yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.

Mgeni Rasmi katika Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Yahaya Nawanda (aliyevaa Skafu) akitoka akikagua vipando kwenye banda la kilimo la Halmashauri ya Wilaya ya Meatu yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.



Muonekano wa bidhaa na vipando mbalimbali zilizozalishwa na kustawishwa kwenye Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, kwenye banda la kilimo la Halmashauri ya Wilaya ya Meatu katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Msoleni Dakawa pamoja na baadhi ya wananchi wakiwa kwenye banda la Halmashauri hiyo lenye bidhaa mbalimbali za Wajasiriamali katika Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane 2022, yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu yaliyoanza rasmi tarehe 01 Agosti 2022 na kuhitimishwa tarehe 08 Agosti 2022.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.