• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu awataka Wakurugenzi kuandaa Mipango Mikakati ya Halmashauri

Imewekwa: May 30th, 2017

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri Mkoani Simiyu kuandaa Mipango Mikakati katika Halmashauri zao.

Sagini ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku tatu ya uandaaji wa Mipango mikakati ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Mkoani Simiyu yanayofanyika wilayani Busega, chini ya Mpango wa Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (PFMRP).

Amesema wakurugenzi wote wahakikishe wanatumia rasilimali zilizopo katika maeneo yao kuhakikisha kuwa wanakamilisha uandaaji wa mipango mikakati hiyo.“ Niwaombe Wakurugenzi Watendaji kuepuka visingizio vya kutokuwa na fedha kutekeleza jambo hili na badala yake mjipange kwa kutumia rasilimali tulizonazo” amesema.

Aidha, amesema Mpango Mkakati ni muhimu kwa kila Halmashari kwa kuwa unasaidia Halmashauri kufikia malengo ya kuanzishwa kwake na kuboresha utoaji huduma za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela  amesema mafunzo hayo yatawasaidia wao kama viongozi na watendaji wengine katika Halmashauri zao kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo zikiwemo za uanzishwaji  na uendeshaji wa viwanda kimkakati.

Wakati huo huo Katibu Tawala huyo amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kutenga maeneo ili kuwezesha utekelezaji wa Sera ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda Mkoani Simiyu.

Mafunzo ya uandaaji wa Mipango mikakati ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri) yamewahusisha Wakurugenzi, Wataalam wa Idara ya Kilimo, Fedha, Mipango na Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa huo (Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Busega, Itilima, Maswa, Meatu na Halmashauri ya Mji Bariadi).

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.