• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Katibu Mkuu Eng. Iyombe atoa neno zito mkutano mkuu ALAT

Imewekwa: September 24th, 2018

Katibu Makuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Mussa Iyombe ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanajitathmini katika utendaji kazi wao hususani katika kuihudumia jamii.

Mhandisi Iyombe ameyasema hayo wakati akitoa mada kwenye Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) nchini ulioanza leo katika ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete jijini Dodoma uliowashirikisha Mameya, Wenyeviti na Wakurugenzi wa Halmashauri zote Nchini.

Mhandisi. Iyombe amewaagiza viongozi hao kuhakikisha wanajibu hoja za Mkaguzi Mkuu wa Serikali pamoja na maelekezo ya Kamati za Bunge kwa wakati ili kila Halmashauri iweze kupata hati safi.

“Serikali imekuwa ikitoa maagizo kuhusu kuhakikisha kila Halmashauri nchini inajibu hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali lakini bado kuna Halmashauri nyingi hazijafanya hivyo, naagiza tena kuwa kila Halmashauri kuacha kulimbikiza hoja za wakaguzi na zihakikishe zinajibiwa kwa wakati” Amesisitiza Mhandisi Iyombe.

Wakati huohuo amewataka viongozi hao kuhakikisha wanafanyakazi kwa ushirikiano na kuacha tabia ya kuwagawa watumishi kwa maslahi binafsi badala ya kuangalia maslahi ya jami jambo linalo kwamisha shughuli za jamii

“Ushirikiano mdogo kati ya Wakuu wa Wilaya,Mameya/Wenyeviti wa Halmshauri na Wakurugenzi unachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo katika Halmashauri nyingi nchini hivyo ni vyema wakafuata sheria na taratibu katika kufanya maamuzi katika utendaji kazi wao.

Ameendelea kufafanua kuwa kuna baadhi ya Halmashauri wanawagawa watumishi na kuleta majungu katika utendaji kazi wao jambo ambalo linasababisha kurudisha nyuma maendeleo katika Halmashauri na kushindwa kutoa huduma bora kwa jamii.

“Inasikitisha kukuta kuna watumishi wanaomsikiliza Meya/ Mwenyekiti na wengine kumsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri jambo hili si sahihi kwa kuwa huwezi kuongoza Halmashauri kama hakutakuwa na ushirikiano katika utendaji kazi’ Anasisitiza Iyombe

Hata hivyo amesisitiza kufuata sheria na taratibu katika kumuazimia mtumishi kwa kuwa upo utaratibu wa kufuata kama Mkurugenzi hatoshi kwenye nafasi yake kupunguza migogoro ya kiutumishi

Amewataka viongozi hao kuhakikisha wanasimamia Mapato na matumizi ya Halmashauri na kutoa nafasi kwa watumishi kwa kuwasikiliza kero zao lengo likiwa ni kujenga mahusiano mazuri katika utendaji kazi wao

“ Tengeni muda wa kuwasikiliza kero za watumishi na wananchi inasikitisha mtumishi anakuja mpaka Wizarani kufuatilia kero ambayo ingeweza kutatuliwa katika ngazi ya Halmashauri naagiza kero zote zitatuliwe katika ngazi ya Halmashauri.“Anasema Iyombe,

Aidha amewaonya Wakurugenzi kutokusita kuwachukulia hatua maafisa Mipango wote nchini wanaoshindwa kuandika maandiko ya miradi ya maendeleo ya kuzisaidia Halmashauri zao kwa ajili ya kuongeza vyanzo vya mapato.

Anaandika Angela Msimbira OR-TAMISEMI

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.