• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Kati ya Ajira 16,676 Zilizotangazwa na Serikali, Meatu Yanufaika na Ajira 109

Imewekwa: June 26th, 2022

Benton Nollo, Meatu

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ni miongoni mwa Halmashauri 185 nchini zilizonufaika na ajira 16,676 ambazo zimetangazwa na Serikali leo tarehe 26 Juni 2022 ikiwa imepangiwa Watumishi 109 ambapo kati yao Watumishi wa Afya ni 58 na Walimu ni 51 (Elimu Sekondari Walimu 34 na Elimu Msingi ni Walimu 17).

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashunga (Mb) amesema katika kada ya afya Wataalamu 6,876 kati yao wanawake ni 3,217 sawa na asilimia 46.8 na wanaume 3,659 sawa na asilimia 53.2 waliomba na kukidhi vigezo wamepangiwa vituo vya kazi huku nafasi 736 za Madaktari wa Meno 59, Matabibu Meno 43, Matabibu Wasaidizi 244, Wateknolojia Mionzi 86 na Wauguzi ngazi ya Cheti 313 zikikosa waombaji wenye sifa.

Waziri Bashunga amebainisha kuwa kwa upande wa Kada ya Elimu, jumla ya walimu 9,800 waliokidhi vigezo wamepangiwa vituo vya kazi ambapo kati yao walimu 5,000 yaani wanawake wakiwa ni 2,353 sawa na asilimia 46.06 na wanaume 2,647 sawa na asilimia 57.94 wamepangiwa shule za Msingi na walimu 4,800 wanawake 1,289 sawa na asilimia 26.85 na wanaume 3,511 sawa na asilimia 73.15 wamepangwa shule za sekondari.

Ajira hizo ni jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi Mahiri wa Rais Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bora ambapo Serikali imeendelea kutoa elimu bila malipo, imeboresha miundo mbinu ya kujifunza na kufundishia pamoja na kuendelea kulipa mishahara ya watumishi wa idara ya elimu huku ikiongeza idadi yao kwa kuajiri.

Vile vile, Serikali inahakikisha afya za Watanzania zinaimarika kwa kuboresha miundombinu ya sekta ya hiyo ambapo kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa shilingi bilioni 1.64 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya vipya viwili ambavyo ni Kituo cha Afya Mwasengela (shilingi milioni 500) na Kituo cha Afya Iramba Ndogo (shilingi milioni 500) na majengo yanayojengwa katika vituo hivyo ni Jengo la Wagonjwa wa Nje – OPD, Maabara, Kichomea Taka, Wodi ya Wazazi na Upasuaji.

Katika Kituo cha Afya Bukundi Serikali ya Awamu ya Sita imeleta shilingi milioni 390 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Wajawazito, Jengo la Upasuaji na Jengo la Maabara (shilingi milioni 300) ilhali shilingi milioni 90 zimeletwa kujenga Nyumba ya Watumishi (3 kwa 1) ambayo ujenzi wake tayari umeshaakamilika.

Kana kwamba haitoshi, Serikali pia imeleta shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Wagonjwa Mahututi – ICU katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu na ujenzi wa jingo hilo upo katika hatua ya umaliziaji.

Pia, Serikali katika kuhakikisha afya za Watanzania zinaimarika wakiwemo wananchi wa Meatu imeendelea kutoa vifaa tiba na kulipa mishahara ya watumishi wa kada ya afya pamoja na kuajiri watumishi wapya kuanzia ngazi ya zahanati.

Aidha, kufuatia ajira za Watumishi zilizotangazwa tarehe 20 Aprili 2022, Watumishi wa Afya na Walimu 16,676 wamepangiwa vituo vya kazi kati ya Watumishi 17,412 waliotakiwa na nafasi 736 zimekosa waombaji wenye sifa hivyo zinatarajiwa kutangazwa tena.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.