• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

JPM atoa kilometa tatu za lami Meatu

Imewekwa: September 10th, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Mawasilianona Uchukuzi kutafuta Mkandarasi wa Ujenzi wa barabara za lami (kilomita tatu ) katika Mji wa Mwanhuzi wilayani Meatu Mkoani Simiyu.

Mhe. Rais Magufuli ameyasema hayo mapema jana wakati akiwahutubia wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Stendi ya Mwanhuzi wilayani Itilima mkoani Simiyu, wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.

Amesema wakati akiwa Waziri wa ujenzi aliahidi ujenzi wa barabara hiyo Waziri wa ujenzi Mawasiliano na uchukuzi ahakikishe anamtafuta Mkandarasi ili aanze kufanya kazi hiyo mwezi huu Septemba 2018, ili ahadi hiyo aliyoitoa kwa wananchi wa Meatu itimie.

“Wakati nilipokuja hapa nikiwa Waziri wa Ujenzi niliahidi ujenzi wa kilomita tatu za lami, nimeshaangaa sana kuona hizo kilomita hazijajengwa, nakuagiaza Waziri wa Ujenzi kabla mwezi huu haujaisha nimuone mkandarasi anaanza kufanya kazi hapa” alisema

Aidha, Mhe. Rais amewataka wananchi kushirikiana na viongozi wao katika kujiletea maendeleo huku akiwasisitiza kuacha kujichukulia sheria mkononi na badala yake wazingatie sheria za nchi.

Katika hatua nyingine Mhe. Rais Magufuli amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweka mipango itakayowezesha wakulima na wafugaji wanafanya shughuli zao kwa amani.

Awali akitoa salamu za Mkoa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa huo una mpango wa kutambua na kuyapima maeneo ya Wafugaji na kuyawekea miundombinu ili wafugaji waachane na ufugaji waachane na kuhama hama na wafuge kwa tija.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi amesema Serikali inajiandaakufanya usanifu wa awali wa Ujenzi wa barabara ya Bariadi-Itilima-Kisesa-Mwandoya-Ng’oboko-Sibiti  ili kwa baadaye ijengwe katika kiwango cha lami.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anaendelea na ziara yake ya siku tatu mkoani Simiyu, ambapo Septemba 10 amesalimia wananchi katika maeneo mbalimbali ikiwemo Lagangabilili Itilima, Kisesa, Mwandoya, mkutano wa hadhara Mwanhuzi na kufungua majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39.

Mwisho.





Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.