• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

IMANI POTOFU YAKEMEWA CHANJO YA KIZAZI MEATU

Imewekwa: April 25th, 2018

Na Linus R. James( Meatu)

“Kama kuna jambo lolote baya  basi Serikali yetu ya Magufuli haiwezi kuthubutu kulileta kwa wananchi”. Hayo yamesemwa na Mh Mkuu wa Wilaya Dk. Joseph Chilongani katika uzinduzi wa chanjo ya kansa ya shingo ya kizazi katika Wilaya ya Meatu.

“Hili sio jambo la kuzuia uzazi bali ni kuzuia ugonjwa unaotokana na uzazi” aliongeza Chilongani. Katika hotuba yake  Mkuu wa Wilaya huyo aliwapongeza watumishi wa Wilaya ya Meatu, makundi mbali mbali ikiwemo makundi ya wawakilishi wa dini, vyama vya siasa na waratibu wa mradi wa chanjo.

Aliwahimiza waendelee kulitangaza hili suala kwa mtazamo chanya kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutumia lugha njema na kutanguliza uzalendo wakati wa kutoa huduma.

Awali akifungua zoezi kaimu Mganga Mkuu Halmashauri  ya Wilaya ya Meatu Dk. Adam Jimisha alitoa taarifa fupi ya chanjo ambapo alisema kuwa Chanjo hii ni endelevu na ni zoezi la kitafa.

Kaimu Mganga Mkuu alisema kuwa chanjo hii haina madhara yoyote kwani imefanyiwa majaribio mbalimbali na shirika la afya duniani (WHO) ambapo hapa nchini majaribio yamefanyika katika mkoa wa Kilimanjaro. Pia alisema zoezi hili ni la kitaifa na lilizinduliwa rasmi Mkoa wa Dar es salaam tarehe 10/04/2018 ambapo kwa Wilaya ya Meatu jumla ya wasichana 11966 wanatarajiwa kupewa chanjo kwa mwaka. Pia alisema kuwa chanjo hii itatolewa bure katika vituo vya afya kwa awamu mbili yaani awamu ya kwanza na awamu ya pili ni baada ya miezi sita tangu msichana atakapochomwa chanjo ya kwanza.

Naye kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ndugu Gervas Amata wakati akimkaribisha mwenyekiti wa Halmashauri alisisitiza kuwa suala hili limekuja wakati muafaka kuokoa vifo kwa wanawake.

“ Wakina mama ndio kila kitu, ndio wazazi, walezi lakini wakina mama ndio walimu na washauri wa mambo yetu katika ngazi ya familia na jamii, tukiokoa wakina mama tumeokoa taifa” alisema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Gervas Amata.

Aliwahimiza wananchi kuwa wananchi wakiacha na kulipuuza zoezi hili matokeo yake siku za baadaye tutapoteza wanawake kwa vifo mbali mbali itakayopelekea kupoteza nguvu kazi ya taifa.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri Mh.Pius Z  Machungwa alisema kuwa chanjo hii katika Wilaya ya Meatu itakua msaada mkubwa katika kujenga afya za wakazi hususani wanawake ambapo pia alihimiza kuwa hili sio jambo baya na chanjo haina madhara kwa wananchi hivyo aliwasihi wazazi wawaruhusu watoto wao wajitokeze kwa wingi kupata chanjo.

Zoezi hili lilitanguliwa na maandamano ya wanafunzi kutoka shule za serikalini nne na binafis moja ambazo ni Mwanhuzi shule ya msiingi, Mshikamano shule ya msingi, Panaeli shule ya msingi  Kimali Sekondari na Meatu sekondari na yalihitimishwa katika viwanja vya Mwanhuzi S/M.

 Kama ishara ya uzinduzi Mh Mgeni rasmi ndugu Chillongani alikata   utepe na baadhi ya wasichana walipewa chanjo mbele ya mgeni rasmi na wageni waalikwa.

 Aidha zoezila chanjo  lilianza kutolewa sambamba  katika hospitali ya Wilaya jengo la RCH na litakua ni endelevu kwa wasichana kuanzia miaka tisa lakin kwa kuanza litaanza na wenye umri wa miaka 14 maelekezo mengine yatatolewa kwa wananchi hapoa baadae.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.