• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

DC, DED wahimiza ufanisi sekta ya afya Meatu

Imewekwa: May 7th, 2018

Na Linus R. James - Meatu

Mkurugenzii Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ndugu Fabian Manoza amewahimiza wafanyakazi wa sekta ya afya kujituma katika kutekeleza majukumu yao ikiwa ni njia ya kuimarisha huduma hiyo pamoja na kuwezesha kufanya vizuri katika miradi mbali mbali inayoendelea ndani ya Wilaya.

Akizungumza mapema  ndugu Manoza  leo hii katika ufunguzi wa mafunzo ya  huduma ya afya ya mfuko wa jamii CHF iliyoboreshwa) amehasa wenyeviti wa kamati za afya katika ngazi ya zahanati na vituo vya faya kuwa wawe makini na waadilifu wakati wanatekeleza miradi yao pamoja hasa kuisimamia kuhakikisha kuwa inakua ni ya kuleta tija katika jamii yao.

“Pesa zote zinazolenga uboreshaji wa afya kwa ngazi ya kijiji, zinaletwa kwenye zahanati lakini wenyeviti mmeshindwa kuzisimamia, sasa ivi mnaingiziwa pesa za basket, pesa za RBF, pamoja na CHF, pesa zote mnazo nyinyi lakini wenyeviti kusema mkae vizuri na kamati zenu mtengeneze mipango mizuri bado hamjaweza kufanya ivo” Alisema Manoza.

Aliwasistitiza kuwa mda wanapokosa pesa wanalalamika lakini zinapoletwa wanashindwa kuonesha matokeo mazuri kwa wananchi.

“Kwa hiyo mimi niwatake mwende mkarekebishe kasoro zinazojitokeza, kinyume cha hapo serikali itaona hakuna maana ya kuleta pesa” Alisisitiza mkurugenzi

Naye katibu tawala wa Wilaya Bi Veronica S. Kinyemi aliwasisitiza washiriki kuwa makini wakati wa mafunzo ili wapate uelew na wakalete ufanisi kwenye vituo vyao.

”Hapa ni makao makuu ya wilayapana mambo mengi sasa isiwe badala ya kuhudhuria mafunzo wewe kila saa na simu nje, mara unaenda benki mara sijui kuonana na nani kiasi kwamba haya mafunzo usiyapate kama yalivyotarajiwa” Alisema Bi Veronica

Akifungua mafunzo, Mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dk. Joseph  Chilongani alisema  kuwa yeye ni dokta(mtabibu) kwa taaluma na kuwaambia kuwa anaelewa machungu ya mgonjwa anapoenda kupata huduma ya matibabu.

“Mimi niseme mmekuja kwenye CHF inayoboreshwa kwa sababu hii iliyopo haijafanya vzuri ivyo tunataka CHF inayofanya vizuri” Alisisitiza Mkuu wa Wilaya.

Aliwahimiza pia kuacha mazoea na wabadilike wafanye kazi kwa weledi ili kuhakikisha huduma inayotarajiwa kwa wananchi ipatikane ambapo pia alitoa maagizo kuwa zahanati amabazo hazifanyi kazi zishughulikiwe haraka ili wananchi wapate huduma ya afya iliyoboreshwa.

“Unaweza ukaugua ukajikuta mfukoni huna pesa lakini kama una bima utahudumiwa kwa sababu tayari ulishachangia” Alidokeza.

Lakini aliwahimiza wenyevti kusimamia kwa ufanisi kuboresha huduma ili wananchi wahamasike kujiunga na bima ya afya.

Mafunzo hayo ya CHF iliyoboreshwa ambayo katika Wilaya ya Meatu yameanza leo kwa ngazi ya Zahanati, vituo vya afya na hospitali yanatarajiwa kuchukua siku tatu yakifuatiwa na mafunzo ngazi ya vijiji ambapo yatahusisha maafisa wasajiri(enrollment officers) ambao watachaguliwa katika jamii kulingana na mwongozo uliotolewa,aidha yatafuatiwa na ufundishaji pia katika ngazi ya vijiji kwa maafisa usajili watakaoteuliwa kulingana namwongozo uliotolewa.

 Aidha baada ya ufunguzi huo  mkurugenzi wa Wilaya liambatana na wakuu wa Idara mbali mbali za Wilaya hiyo kukagua miradi mbali mbali inayotekelezwa ikiwemo uboreshaji wa Hospitali ya Wilaya  unaohusisha ujenzi wa maabara, chumba cha upasuaji“theater” pamoja na wodi ya wazazi, piaa kukagua ukarabati wa zahanati.


Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.