• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

DC – Chilongani aongoza Hafla ya kuwapongeza wahitimu wa Diploma ya elimu ya watu wazima Wilayani Meatu

Imewekwa: February 2nd, 2019

Na Linus R. James - MEATU DC

Mkuu wa wilaya ya Meatu Dk. Joseph E. Chilongani ameongoza hafla ya kuwapongeza wahitimu katika kituo cha elimu ya watu wazima ngazi ya stashahada kituo cha Meatu iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu jana jioni.

Dk Chilongani ambaye  alikua mgeni rasmi wa hafla hiyo alionekana kufurahishwa sana na tukio hilo ambapo alisema ni jambo jema sana la kihistoria tangu kuanzishwa kwa wilaya ya  Meatu.

“ Nyinyi mmekua chachu nzuri katika  Wilaya yetu mnaona watu wamekuja na familia zao leo  na nisingependa mkomee hapa, ningependa muendelee elimu ya juu Zaidi” Alisema Mkuu wa Wilaya.

Pia  mkuu wa wilaya alisema kuwa kukosa majengo haimaanishi mambo hayafanyiki ambapo aliahidi kushirikia na  Idara ya elimu ili kufanya mazungumzo ya kuwa na kozi nyinginezo ikiwa ni pamoja na shahada..

“Fursa ya kujiendeleza ipo kama mnavyojua nchi yetu inatusisitiza maendeleo ya viwanda, maendeleo ya uchumi, na haya yote hayaji pasipokkuwa na wasomi”. Alisisitiza  Mkuu wa Wilaya.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mtendji wa Wilaya ya Meatu Ndg. Gervas Amata alisema kuwa kwa kuwa mtu anapopiga hatua nyingine ya kielimu anahitaji stahiki ikiwa ni pamoja na mishahara na vituo vya kazi alimwambia mgeni rasmi kuwa stahiki hizo zitatekelezwa kwa mujibu wa utarabibu na ofisi yake itajitahidi kuzifanyia kazi changamoto mbali mballi zinazojitokeza katika kituo hicho cha elimu ya watu wazima.

Naye mkuu wa Idara ya Elimu Ndg. Mshana Kawia akimkaribisha mgeni rasmi  licha ya kumshukuru mkurugenzi mtendaji kwa kukubali kituo kianzishwe na kutoa chakula kipindi chote cha masomo aliweza kubainisha mikakati iliyopo katika kituo hicho ambapo alisema kituo kina mkakati wa kutoa elimu ngazi ya shahada kwa kipindi cha baadae. Pia alibainisha faida ambazo wanazipata wanafunzi wanaosoma katika Kituo cha elimu ya watu wazima hususani walimu,

“ Kituo hiki kina faida kubwa kwa sababu kwanza walimu hawa wanasoma kipindi cha likizo, kwa hiyo walimu wanapata mda wa kufundisha, kutunza familia zao na kufanya shughuli za ujasiriamlai”. Alisema Ndg. Mshana.

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu chini ya Idara ya Elimu msingi katika Jitihada za kuboresha taaluma ya walimu ilianzisha kituo cha stashahada ya elimu ya watu wazima mnamo mwezi Disemba 2016 ambapo kituo kilifunguliwa rasmi na mkurugenzi mtendaji tarehe 10/04/2017 ambapo kilianza na wanafunzi 32 wote wakiwa ni waalimu wa shule mbali mbali wilayani meatu ambapo mwaka 2019 wanafunzi 29 wamehitimu  masomo yao.

Akisoma risala kwa niaba ya Wahitimu mwanafunzi alisema kuwa  kati ya mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na walimu kuongeza  umahili kazini

“Moja ya mafanikio ya kituo cha elimu ya watu wazima hapa Meatu ni kuwepo kwa wahitimu wapatao 29 wenye diploma ya elimu ya watu wazima, kwa hiyo Idara ya elimu imeongeza watumishi wenye umahiri wa kutosha”  alisema muhitimu

Kituo hiki kinakabiriwa na changamoto mbali mbali zikiwemo kutokua na majengo yake chenyewe pamoja na kutokuwa na maktaba kwa aili ya kupata marejeo ya masomo.

MWISHO

Picha zaidi bofya hapa


Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.