• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Dakawa: Hongereni, Kazi Mnayofanya Kubwa

Imewekwa: January 13th, 2023

Na Benton Nollo, Mwanhuzi

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Msoleni Dakawa amewapongeza Walimu kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kufundisha wanafunzi na usimamizi mzuri wa miradi inayopelekwa katika maeneo yao.

Dakawa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya utiaji saini Mikataba ya Utendaji Kazi kati ya Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Wilaya ya Meatu, Elizabeth Kiraya pamoja na Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Wilaya ya Meatu, Hadija Rajabu na Maafisa Elimu Kata wote 29 katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo tarehe 13 Januari 2023.

Mkurugenzi Dakawa amesema pamoja na kwamba zipo changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili walimu hao katika maeneo yao lakini ameeleza kuwa pamoja na yote hayo Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuzifanyia kazi.

"Madharani kwa mwaka huu wa fedha (2022/2023) Halmashauri yetu tumeletewa fedha zaidi ya shilingi milioni 980 kwa ajili ya kulipa madai (arrears) ya watumishi 750 kwa mara moja, hili siyo jambo dogo." Anasema Dakawa na kuongeza;

"Lakini pia katika mwaka huu huu wa fedha, Mheshimiwa Rais Sami ameridhia watumishi 499 kupandishwa vyeo...pia, katika miradi ya elimu tumeletewa shilingi bilioni 1.48 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 74...kana kwamba haitoshi kupitia program ya EPforR tumeletewa shilingi milioni 190 katika Shule ya Sekondari Ngh'oboko...ndiyo maana nasema tuna kila sababu ya kumpongeza Rais wetu na sisi sote kwa kazi nzuri tunayofanya."

Aidha, Dakawa amewataka walimu na watumishi wengine wote katika Halmashauri hiyo kuepuka utoro kazini na kutokaa katika vituo vya kazi na badala yake wawajibike ipasavyo katika utekelezaji wa majukumu yao ili kuinua elimu na utoaji wa huduma bora kwa wananchi wa Meatu.

Pamoja na Maafisa Elimu Kata 29 waliohudhuria kusaini mikataba hiyo, kikao hicho pia kilihudhuriwa na Wakuu wa Shule 29 na Walimu Wakuu 122 wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.