• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Dakawa Aongoza Maziko

Imewekwa: May 14th, 2022

Na Benton Nollo, Meatu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Msoleni Dakawa (pichani aliyevaa shati jeupe) tarehe 13 Mei 2022 ameongoza mamia ya waombolezaji wa Kijiji cha Ming'ongwa kwenye mazishi ya Njile Ngagaja (35) aliyefariki baada ya kukanyagwa na tembo waliovamia kijiji hichousiku wa kuamka tarehe 13 Mei 2022.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Frank Mganga amethibitisha kutokea kwa kifo cha mwananchi huyo wakati akipatiwa matibabu katika Kituo cha Afya Mwandoya alipofikishwa akiwa na hali mbaya baada ya kujeruhiwa vibaya na tembo huyo tumboni na miguuni.

Marehemu Ngagaja ni mkazi wa Kitongoji cha Ipililo, Kijiji cha Ming'ongwa Kata ya Sakasaka wilayani humo.

Tembo hao walivamia Kijiji hicho majira ya saa 4 usiku tarehe 12 Mei 2022 wakitokea Pori la Akiba la Maswa (Maswa Game Reserve) ambapo pamoja na kusababisha kifo kwa mwananchi huyo pia tembo hao wamesababisha taharuki na uharibifu mkubwa wa mali za wananchi ikiwemo mazao katika maeneo hayo.

Akitoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki waliofiwa Dakawa amewasilisha salamu za Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani humo, Luhaga Mpina kwa kuwaeleza kwamba amepokea kwa majonzi na masikitiko makubwa tukio la msiba huo na kuahidi kwamba kwa kuwa anaendelea na vikao vya Bunge la Bajeti jijini Dodoma ataonana na Waziri wa Maliasili na Utalii ili hatua mahususi na za haraka kudhibiti tembo hao na wanyama wengine waharibifu zichukuliwe.

Hata hivyo, Mbunge huyo baada ya kupatiwa taarifa hiyo ameshiriki kugharamia gharama za hospitali na  mazishi ya mwananchi huyo.

Tatizo la wananchi kuvamiwa na tembo katika Wilaya ya Meatu hasa Jimbo la Kisesa, limekithiri licha ya kuwepo kwa  jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali kukabiliana na changamoto hiyo.

Hata hivyo, tarehe 04 Februari 2022 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shemsa Mohamed alifikisha kilio hicho mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika Mji Mdogo wa Lamadi wilayani Busega akiwa njiani kuelekea mkoani Mara, ambapo Rais Samia aliiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuanzisha vituo maalum vya  kufukuza tembo katika vijiji vinavyopakana na hifadhi hiyo na kama hawana askari waombe kibali ili waongezewe askari.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Diwani wa Kata ya Sakasaka, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kisesa pamoja na Maafisa kutoka Pori la Akiba la Maswa.

Wananchi wa Vijiji 14 kati ya 18 vinavyopakana na Pori la Akiba la Maswa vipo Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu.

Vijiji hivyo ni Mbugayabhanya, Mwamashimba, Semu, Nyanza, Butuli, Sakasaka, Bulyandulu, Mwamhongo, Ng'hanga, Matale Ming'ongwa, Mwanindwa, Mwasengela na Tindabuligi.


Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.