• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Maono
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
        • Misitu
        • Wildlife Management
        • Ardhi
    • Vitengo
      • Ununuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Mtaa
    • Vijiji
  • Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Town Planning and Environmental Committee
      • AIDS Control Committee
      • Ethics Committee
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti Wa Halmaashauri
  • Miradi
    • Maandiko ya Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayotekelezwa
      • TASAF
      • LVEMP II
      • Uzalishaji wa Mbegu za Pamba
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • District Profile and Maps
    • Acts and Regulations
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Fomu
    • Taarifa
    • Circulars
    • Dokumbenti Mbali mbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Hotuba

Dakawa Aongoza Maziko

Imewekwa: May 14th, 2022

Na Benton Nollo, Meatu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Msoleni Dakawa (pichani aliyevaa shati jeupe) tarehe 13 Mei 2022 ameongoza mamia ya waombolezaji wa Kijiji cha Ming'ongwa kwenye mazishi ya Njile Ngagaja (35) aliyefariki baada ya kukanyagwa na tembo waliovamia kijiji hichousiku wa kuamka tarehe 13 Mei 2022.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Frank Mganga amethibitisha kutokea kwa kifo cha mwananchi huyo wakati akipatiwa matibabu katika Kituo cha Afya Mwandoya alipofikishwa akiwa na hali mbaya baada ya kujeruhiwa vibaya na tembo huyo tumboni na miguuni.

Marehemu Ngagaja ni mkazi wa Kitongoji cha Ipililo, Kijiji cha Ming'ongwa Kata ya Sakasaka wilayani humo.

Tembo hao walivamia Kijiji hicho majira ya saa 4 usiku tarehe 12 Mei 2022 wakitokea Pori la Akiba la Maswa (Maswa Game Reserve) ambapo pamoja na kusababisha kifo kwa mwananchi huyo pia tembo hao wamesababisha taharuki na uharibifu mkubwa wa mali za wananchi ikiwemo mazao katika maeneo hayo.

Akitoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki waliofiwa Dakawa amewasilisha salamu za Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani humo, Luhaga Mpina kwa kuwaeleza kwamba amepokea kwa majonzi na masikitiko makubwa tukio la msiba huo na kuahidi kwamba kwa kuwa anaendelea na vikao vya Bunge la Bajeti jijini Dodoma ataonana na Waziri wa Maliasili na Utalii ili hatua mahususi na za haraka kudhibiti tembo hao na wanyama wengine waharibifu zichukuliwe.

Hata hivyo, Mbunge huyo baada ya kupatiwa taarifa hiyo ameshiriki kugharamia gharama za hospitali na  mazishi ya mwananchi huyo.

Tatizo la wananchi kuvamiwa na tembo katika Wilaya ya Meatu hasa Jimbo la Kisesa, limekithiri licha ya kuwepo kwa  jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali kukabiliana na changamoto hiyo.

Hata hivyo, tarehe 04 Februari 2022 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shemsa Mohamed alifikisha kilio hicho mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika Mji Mdogo wa Lamadi wilayani Busega akiwa njiani kuelekea mkoani Mara, ambapo Rais Samia aliiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuanzisha vituo maalum vya  kufukuza tembo katika vijiji vinavyopakana na hifadhi hiyo na kama hawana askari waombe kibali ili waongezewe askari.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Diwani wa Kata ya Sakasaka, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kisesa pamoja na Maafisa kutoka Pori la Akiba la Maswa.

Wananchi wa Vijiji 14 kati ya 18 vinavyopakana na Pori la Akiba la Maswa vipo Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu.

Vijiji hivyo ni Mbugayabhanya, Mwamashimba, Semu, Nyanza, Butuli, Sakasaka, Bulyandulu, Mwamhongo, Ng'hanga, Matale Ming'ongwa, Mwanindwa, Mwasengela na Tindabuligi.


Matangazo

  • Tangazo la Orodha ya Majina Waliopata Ajira Kada za Afya na Ualimu Juni 2022 June 26, 2022
  • Tangazo la nafasi za Kazi Meatu May 30, 2022
  • Tangazo la Majina ya Waliochaguliwa Kukusanya Taarifa ya Anuani za Makazi na Postikodi March 24, 2022
  • MICHORO YA MAJENGO YA AFYA February 10, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Kati ya Ajira 16,676 Zilizotangazwa na Serikali, Meatu Yanufaika na Ajira 109

    June 26, 2022
  • 'The Heroes' Wakabidhiwa Basi Baada ya Kukopeshwa Milioni 72

    May 20, 2022
  • Dakawa Aongoza Maziko

    May 14, 2022
  • Shillingi 117,467,622 zatolewa kwa ajili ya vijana, wanawake na wenye ulemavu

    October 04, 2021
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.