• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

AMREF yaendelea kuboresha huduma za afya ya Jamii Meatu

Imewekwa: May 6th, 2019

Na Linus R. James ( Meatu DC)

 Shirika la AMREF( Tanzania na Canada) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo  Marie Stopes International,  Deloitte na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wameendelea kuboresha huduma ya afya kwa jamii hususani wazazi kupitia wahudumu wa afya ngazi ya jamii.

Hayo yamebainishwa mapema leo wakati wa makabidhiano ya baiskeli 69 zenye jumla thamani ya shilingi 16, 524,000 za Kitanzania yaliyofanyika katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Meatu.

Akizungumza wakati wa makabidhiano, Afisa Mradi Uzazi na Uzima Ndg. Henericko Ernest  alisema lengo la mradi wa uzazi na uzima ni kuzidi kushirikiana na Wilaya ya Meatu pamoja na wadau wa afya kuhakikisha wanapunguza vifo.

“ Mwaka jana Mwezi wa saba na wa nane tulitoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya vijiji kwa ajili ya kuhamasisha wazazi kuhudhuria kliniki na vituo vya afya pamoja na masuala ya lishe na leo tunakabidhi baiskeli hizi ili yale waliyoyapata katika mafunzo yaweze kufanyiwa utekelezaji kikamilifu ” Alisema Ndg. Henericko.

Afisa mradi huyo alisema kuwa mbali na kutoa mafunzo walihahidi kusaidia vitendea kazi mbali mbali, vikiwemo baiskeli, maboresho ya huduma za dharula yaani wodi ya wazazi na upasuaji,  pamoja na kuboresha miundombinu ya maji katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Naye Kaimu Mganga mkuu wa hospitali ya Wilaya Dr. Frank Mganga akitoa shukrani kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji alisema kuwa baikeli hizi zitaleta chachu

“Hizi Baiskeli 69 Kituo cha afya Mwandoya kitapata baiskeli 40, Zahanati ya Ng’hoboko 16 na Imalaseko 13, baiskeli hizi zimezingatia idadi ya wahudumu waliopo katika vituo husika katika ngazi ya afya ivyo naamini zitaleta chachu katika kuboresha na kuimarisha huduma ya afya kwa wananchi ndani ya Wilaya ya Meatu” Alisema Dr. Mganga.

Aidha baada ya makabidhiano katika halmashauri ya wilaya baiskeli hizo zmesambazwa kwenye vituo husika na zitakua chini ya usimamizi wa vituo husika, uongozi wa kijiji chini ya ofisi ya Mganga Mkuu wa wilaya.

Ikumbukwe kuwa mradi wa Afya na uzima unatekelezwa katika mkoa wa Simiyu kwa kipindi cha miaka miine katika Wilaya zote za Simiyu ambapo ulianza mwaka 2017 na unatarajia kukamilika mwaka 2020.

MWISHO

Picha zaidi Bofya hapa

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.