• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

TASAF

HALMASHAURI YA WILAYA YA MEATU

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA TASAF AWAMU YA TATU

Mpango wa TASAF wa Kunusuru Kaya Maskini

 

1.0 Utangulizi

Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini chini ya TASAF awamu ya III ulianza katika Halmashauri ya Meatu tarehe 17/07/2014 kwa kujenga uelewa wadau mbalimbali juu ya Mpango huo. Zoezi la kutambua kaya maskini liliendeshwa kuanzia tarehe 21/07/2014 hadi 10/09/2014 katika vijiji 64 vilivyoteuliwa kushiriki katika mpango huu ambapo kaya maskini 7,020 zilitambuliwa. Zoezi hilo lilifuatiwa na zoezi la kuhakiki na kuandikisha kaya hizo kuanzia tarehe 13/10/2014 hadi 16/11/2014 ambapo kaya 5,810 ziliandikishwa. Hatimaye kaya 5,800 ziliidhinishwa na TASAF makao makuu kwa ajili ya kupokea malipo ambayo yamekuwa yakifanywa kwa vipindi vya miezi miwili miwili kuanzia Julai 2015.


2.0 Idadi ya walengwa walionufaika na wasionufaika

Malipo ya walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini yamefanyika kwa vipindi vitano tofauti ambapo jumla ya shilingi 1,040,409,174/= zimelipwa. Vipindi hivyo vya malipo ni Julai & Agosti 2015, Septemba & Oktoba 2015, Novemba & Desemba 2015, Januari & Februari 2016, na Machi & Aprili 2016 .

Jedwali hapa chini linaonesha idadi ya kaya zilizoizinishwa, zinazonufaika na zisizonufaika katika vipindi vyote vya malipo

KIPINDI CHA MALIPO

IDADI YA

KAYA ZILIZIIDHINISHWA

IDADI YA KAYA ZILIZOLIPWA

IDADI YA KAYA AMBAZO HAZIKULIPWA

Julai & Agosti 2015

5,800

5,634

166

Septemba & Oktoba 2015

5,800

5,702

98

Novemba & Desemba 2015

5,800

5,636

161

Januari & Februari 2016

5,800

5,700

100

Machi & Aprili 2016

5,800

5,479

321


2.1 Sababu za baadhi walengwa kutolipwa:

- Kutojitokeza kwa walengwa na kushindwa kutuma wawakilishi kwa ajili ya kuwapokelea fedha zao siku za malipo.

- Kufariki dunia kwa mlengwa asiye na mtegemezi.

- Kusimamishwa kwa malipo baada ya mlengwa kutambuliwa na mkutano maalum wa kijiji mwezi Februari 2016 kuwa hana sifa za kuwa mlengwa wa Mpango.


3.0 Manufaa ya Malipo kwa Walengwa

- Kaya maskini zimenufaika na malipo yanayotolewa na Mpango na zimeweza kufanya mambo mbalimbali kwa ajili ya kuboresha hali ya maisha yao ikiwemo haya yafuatayo:

- Kutosheleza mahitaji ya shule kwa watoto kama kununua sare za shule, vitabu, daftari na kalamu.

- Kuimarisha afya ya familia kwa kulipia gharama za matibabukujiunga na Mfuko wa afya ya jamii (CHF).

- Kuboresha makazi ya familia kwa kununua vifaa vya ujenzi wa nyumba kama vile mabati, misumari na saruji.

- Kuanzisha miradi midogo midogo ya ujasiriamali kama vile ufugaji wa mbuzi na kuku wa kienyeji kwa ajili ya kuboresha lishe na kuinua kipato cha familia.

- Kununua mahitaji ya familia kama vile mavazi, sabuni na chakula (mfano, sukari, majani ya chai, chumvi, mafuta ya kupikia na nyama).


4.0 Changamoto

- Baadhi ya majina ya watoto wanaotakiwa kutimiza masharti ya elimu na afya yanayotumwa Halmashauri kutoka TASAF makao makuu kwa ajili ya kuhakiki mahudhurio kugundulika kuwa sio majina ya watoto wa shule au vituo vya afya wanakotakiwa kuhudhuria. Taarifa hizi zimefikishwa kwa wahusika kwa ajili ya marekebisho.

- Kaya nyingi zilizotajwa katika mikutano ya vijiji ya kubaini kaya zisizo na sifa iliyofanyika Februari 2016 kujitokeza kwa ajili ya malipo na kuonyesha kutokubaliana na maamuzi ya mikutano hiyo ya vijiji. Kaya hizo zitatembelewa kwa ajili ya uhakiki.

- Idadi ya kaya zinazoishi katika lindi la umaskini katika Halmashauri ya Meatu bado ni kubwa. Kaya hizi zipo katika vijiji vinavyohudumiwa na Mpango na pia katika vijiji ambavyo bado havijafikiwa na Mpango. Orodha ya vijiji ambavyo bado havijafikiwa na Mpango ilitumwa TASAF makao mwaka 2015.

 

5.0 Hitimisho

Utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya maskini unaendelea vizuri katika Halmashauri ya Meatu. Jumla ya shilingi 1,040,409,174 zimelipwa kwa walengwa na wameweza kunufaika kwa kiasi kikubwa.


Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.