• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Wazir Tizeba: Waandaahi nane nae andaeni maonesho yatakayosaidia kuleta Tija kwa wananchi katika uzalishaji

Imewekwa: August 3rd, 2018

Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba amewataka Waandaaji wa Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nanenane hapa nchini kuhakikisha kuwa kuanzia mwaka 2019 wanaandaa maonesho hayo katika sura mpya itakayoleta mabadiliko chanya kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ili waweze kuzalisha kwa tija.


Anaandika Stella Karinga - Simiyu.

Waziri Tizeba ameyasema hayo Agosti 03, 2018 katika Uwanja wa Nanenane Kanda ya Ziwa Mashariki, uliopo Nyakabindi Bariadi, wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018 yanayofanyika Mkoani Simiyu.

Amesema ni vema waandaaji hao wakatoka katika maonesho ya mazoea ya kuwaonesha wakulima na wadau  vipando mbalimbali pasipo kuwapa elimu ya namna yakufikia uzalishaji wanaouona katika maonesho, badala yake maonesho hayo yatumike kuwafundisha wananchi na kubadilishana uzoefu.

“Kuanzia nanenane ya mwaka huu na zinazofuata, wandaaji wazipe sura mpya hata tunapowaomba wadau mbalimbali kuchangia maandalizi wawe wananamini kuwa tutakachokifanya kitaleta  mabadiliko chanya kwa wakulima, wafugaji na wavuvi wa nchi hii”alisema Tizaba.

 

Aidha, Dkt. Tizeba amekubaliana na mpango wa viongozi wa Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kufanya maonesho kila baada ya miezi mitatu katika Uwanja wa Nyakabindi ili kuwapa fursa wananchi ya kuendelea kujifunza badala ya kusubiri kila wiki ya nanenane kila mwaka.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Mkoa huo na kanda ya Ziwa ya Mashariki ni kuendelea kufanya maonesho Teknojia za Kilimo  Biashara katika Uwanja wa Nyakabindi jambo ambalo litawapunguzia Watanzania kwenda nje ya nchi kujifunza teknolojia hizo.

“Tutafanya maonesho hapa kila baada ya miezi mitatu, kupitia maonesho yatakayofanyika eneo hili, tutawapunguzia wananchi safari za kwenda nje ya nchi  kufuata teknolojia za kilimo Biashara” alisema Mtaka.

Katika hatua nyingine Mtaka amesema Waoneshaji waliopo Uwanja wa Nanenane Nyakabindi wameomba kuongezewa siku mpaka kufikia Agosti 11 badala ya Agosti 08 kama ilivyo kawaida, jambo ambalo lilikubaliwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Dkt. Charles Tizeba.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amesema matarajio ya viongozi wa Kanda ya Ziwa Mashariki ni kuyafanya maonesho ya nanenane kanda hiyo kuwa mnara wa mafanikio katika sayansi na teknolojia na namna ambavyo kilimo kinachozingatia kanuni bora kinavyochangia mabadiliko chanya ya mfumo wa Watanzania waanotegemea kilimo.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba ametoa wito kwa wananchi kufika Uwanja wa Maonesho ya Nanenane Nyakabindi ili kupata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali kwa kuwa kwa sasa waoneshaji wa teknolojia mbalimbali wapo uwanjani hapo.

  

Maadhimisho ya Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nanenane mwaka 2018 yanayofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu ni ya 25 kufanyika hapa nchini na Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba amesema maonesho hayo yatafanyika miaka mitatu mfululizo, mwaka 2018, mwaka 2019 na mwaka 2020.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.