• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Simiyu kuandaa Mwongozo wa Uwekezaji kwa kila Kijiji

Imewekwa: December 12th, 2018

Na Stella A. Kalinga

Mkoa wa Simiyu umejipanga kuandaa mwongozo wa uwekezaji  kwa kila Kijiji na Mtaa utakaobainisha fursa za uwekezaji zilizopo katika kijiji na mtaa husika katika vijiji vyote 471 na Mitaa 92 ya wilaya zote tano za Mkoa huu, ikiwa ni maandalizi ya utekelezaji wa Falsafa ya Bidhaa Moja Kijiji Kimoja(OVOP) mwaka 2019/2020.

Hayo yamebainishwa Desemba 11, 2018 Mjini Bariadi katika kongamano la kuwajengea uwezo Watendaji wa Vijiji 471, Watendaji wa Mitaa 92, Watendaji wa Kata 130 na Maafisa tarafa 16 juu ya kuibua fursa za uwekezaji kwa ajili ya kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na mtaa, kwa kushirikiana na Wataalam kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ESRF), ambalo pia limewahusisha viongozi na watendaji wa Chama na Serikali ngazi ya wilaya na Mkoa.

Awali akifungua kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Mkoa huu unatekeleza Falsafa ya Bidhaa Moja Wilaya ambayo ilianza baada ya ESRF kufanya utafiti na kuibua fursa 26 ndani ya mkoa na sasa inajipanga kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na kuanza utekelezaji wa Bidhaa Moja Kijiji Kimoja.

"Miaka mitatu ya utekelezaji wa Bidhaa Moja Wilaya Moja imetosha, mwaka 2019/2020 ni Bidhaa Moja Kijiji Kimoja, ESRF watatusaidia kufanya utafiti utakaoonesha kila kijiji kina fursa gani; Mkoa wa Simiyu utakuwa mkoa wa kwanza kwenye nchi hii ambao kila kijiji na mtaa utakuwa na mwongozo unaoonesha fursa za uwekezaji za kijiji au mtaa huo" alisisitiza.

Mtaka ameongeza kuwa mara baada ya kukamilisha mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji, mkoa utaandaa utaratibu kwa kushirikiana na Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) kuona namna ya kuweka teknolojia/mashine zitakazotumika kuongeza thamani mazao ya kilimo, mifugo na mengine yanayopatikana katika kijiji au mtaa husika kulingana na fursa zitakazoainishwa.

Kwa upande wake Mtafiti Mkuu Mshiriki kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF), Prof. Samwel Wangwe amesema mkoa wa Simiyu unafanya vizuri katika kilimo hivyo fursa za kuongeza thamani ya mazao ya kilimo zitakuwa kipaumbe cha kwanza, ikifuatiwa na uwekezaji kwenye miradi itakayoleta maendeleo ya binadamu pamoja na mageuzi katika masuala ya kijamii.

Nao Watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata wamewapongeza viongozi wa Mkoa kwa maono ya kila kijiji na mtaa kuwa na mwongozo wa uwekezaji na kuahidi kusimamia kikamilifu fursa zitakazoibuliwa katika maeneo yao, ili ziweze kuleta mapinduzi ya Kiuchumi kwa wakazi wa Simiyu.

" Nimeupokea vizuri sana mpango wa kila kijiji na mtaa kuwa na mwongozo wake wa uwekezaji, binafsi naahidi kusimamia kikamilifu fursa zote zitakazoibuliwa kupitia mafunzo tuliyopewa leo na tafiti zitakazofanywa na wataalam, ili zilete mapinduzi ya Kiuchumi kwa wananchi na mkoa wa Simiyu kwa ujumla" Twaibu Abdul Rashid, Afisa Mtendaji wa Kata ya Kinamweli wilaya ya Itilima.

"Tunamshukuru sana Mkuu wa Mkoa kuja na wazo hili ambalo tunaamini tukilisimamia vizuri litainua sana mkoa wetu kiuchumi, maana wananchi watakuwa wanafahamu kuwa ni eneo gani katika kijiji au mtaa wao linaloweza kuwainua kiuchumi kupitia uwekezaji watakapotambua fursa za uwekezaji zilizopo" Amina Yusuph Mtendaji wa Mtaa wa Ng'waswale, Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo amesisitiza kuwa ili kufikia malengo ya kuinua mkoa huo kiuchumi ni kuendeleza ushirikiano uliopo katika ya viongozi  wa Chama na Serikali na wananchi.

MWISHO

Zaidi bofya hapa

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.