• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Rc Mtaka aongoza harambee ya ujenzi wa Bweni la Mwanjolo

Imewekwa: September 1st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka ameongoza Harambee ya Ujenzi wa Bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari Mwanjolo Wilayani Meatu ambapo jumla shilingi milioni 84,876,950/= zimepatikana, fedha taslimu ikiwa shilingi 18,776,000/= ahadi 66,100,000/= pamoja na mifuko 253 ya saruji, mbuzi 12  na ng’ombe 3.

Akizungumza na wananchi na viongozi wa Chama na Serikali Mtaka amewapongeza viongozi wa kata ya Mwanjolo kwa jitihada walizofanya kwa kushirikiana na wananchi katika kuhakikisha wanafunzi wa kike wanapata bweni, huku akiwasisitiza wananchi kuona umuhimu wa kuwekeza katika elimu ili kuuweka mkoa huo kwenye ushindani na mikoa mingine.

Aidha, ametoa wito kwa Madiwani wa kata zote mkoani humo kuiga mfano wa Kata ya Mwanjolo ambapo amesema viongozi na wananchi wanapaswa kuona uchungu na kuona haja ya kuwa na mabweni kwa watoto wa kike ili waondakane na vishawishi na changamoto nyingine zinazowakabili ili waweze kufikia malengo yao.

“Madiwani wetu hili jambo waige, haiwezekani hawa wasichana wadogo wanaenda kupanga kwenye vijiji pateni uchungu watoto wa kike wajengewe hosteli, Mungu ametupa ardhi, mifugo, nguvu za kufanya kazi, tukishikamana kama watu wa Mwanjolo, watoto wetu wa kike wote watapata mabweni”

“Mwanjolo wametuamasha, niwaombe waheshimiwa madiwani na viongozi wenzangu kwenye wilaya zote za Mkoa wa Simiyu moto huu uliowashwa hapa Mwanjolo uende kwenye kata zote, tuanze kujenga mabweni ya watoto wa kike wanapofaulu kwenda kidato cha kwanza wakae shule wasitembee njiani wakaanza kupewa lift za baiskeli na bodaboda” alisema Mtaka

Ameongeza kuwa kwa sababu elimu ni kipaumbe cha kwanza cha mkoa ni vema viongozi wote mkoani humo wakaweka dhamira kuwa kufikia mwaka 2020 wanafunzi wa kike wote wanaosoma shule za sekondari mkoani Simiyu wakae bweni.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mhe. Luhaga Mpina ametoa wito kwa Wananchi hususani jamii ya wafugaji kuchangia na kuunga mkono jitihada mbalimbali za maendeleo ya elimu ili watoto wa jamii za kifugaji waweze kusoma katika mazingira mazuri.

Wakati huo huo amewahimiza vijana wanaotoka katika jamii za kifugaji kusoma kwa bidii ili waweze kuzisaidia jamii zao kufuga ufugaji wenye tija utakaowaletea manufaa.

Nao wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Mwanjolo wamewashukuru viongozi na wananchi ambao wamechangia ujenzi wa bweni, ambapo wamesema endapo bweni hilo litakamilika litawasaidia kuondokana na vishawishi mbalimbali vilivyokuwa vikisababisha baadhi yao kupata ujauzito na kushindwa kumaliza masomo yao.

“Kukamilika kwa bweni kutatusaidia kutatua changamoto tunazokutana nazo sisi wasichana hasa suala la mimba, kuna wenzangu nilioanza nao kidato cha kwanza mwaka 2016 hawapo shuleni sasa hivi sababu ya mimba, naamini tukikaa bweni tutakuwa salama  na tutapata muda mwingi wa kujisomea kwa kuwa hatutatembea mwendo mrefu tena”  Eunice Kapombe mwanafunzi Kidato cha Tatu.

Kwa upande wao wazazi na walezi wa baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwanjolo wamesema ujenzi wa bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Mwanjolo utakuwa msaada mkubwa kwa watoto wa kike katika kuwawezesha kufikia kwenye malengo yao,kwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakikatisha masomo kutokana na mimba zinazosababishwa na vishwawishi wanavyopata kwa kutembea mwendo mrefu kwenda shule na baadhi yao kupanga vijijini.

Harambee ya ujenzi wa Bweni la Wasichana Shule ya Sekondari Mwanjolo iliyofanyika Shuleni hapo Agosti 31, 2018,  imehusisha viongozi wa Chama na Serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya ya Meatu, Wadau mbalimbali wa Maendeleo na wananchi, ambapo mpaka kukamilika kwa Bweni hilo jumla ya shilingi 125,024,504.35 zitahitajika.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.