• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Meatu na Iramba zaweka mkakati wa kuboresha mazalia ya samaki ziwa Kitangiri

Imewekwa: January 13th, 2019

Na Linus R. James - Meatu DC

Halmashauri za Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu  na Iramba  Mkoani Singida zimekubaliana  kwa pamoja kuwa na  mikakati ya kuboresha na kutunza  mazalia  ya samaki katika Ziwa Kitangiri ikiwa ni pamoja kufunga ziwa Kitangiri yaani mkakati wa mda mfupi pamoja na kutengeneza sheria ndogo ndogo na Miongozo  ambayo itakakua ni mikakati ya mda mrefu.

Makubaliano hayo yamefanyika jana katika kikao cha pamoja cha ujirani mwema kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Meatu Mkoani Simiyu kikihusisha kamati za ulinzi na usalama, Waheshimiwa madiwani, Wenyekiti wa Halmashauri, Viongozi wa Chama cha Mainduzi , Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndg. Fabian Manoza Said pamoja na wakuu wa Idara na vitengo wa Halmashauri zote mbili.

Akifungua kikao hicho cha Ujirani mwema Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dk. Joseph Chilongani alisema

‘’ Ni jukumu letu sisi viongozi wa Wilaya hizi kuhakikisha tunatunza na kuhifadhi mazingira ya Ziwa Kitangiri ili kutoa fursa samaki wazaliane kwa wingi na wakubwa kwa ajili ya kitoweo kwa jamii na kuwaongezea kipato wananchi kwa ujumla pamoja na kuongeza mapato ya Halmashauri zetu.’’

‘’ Cha msingi Halmashauri wilaya za Iramba Meatu, Igunga na Wilaya ya Kishapu tulikuwa na utaratibu wa pamoja za Kufunga Ziwa Kitangiri kila mwaka lakini hatukuwa mpango mkakati wa pamoja kuamua ni lini ziwa hili litakuwa linafungwa kila mwaka, hata hivyo katika kikao cha Ujirani mwema tuliofanya mjini Shinyanga mwaka juzi tulikubaliana kuhifadhi Ziwa Kitangiri na kupiga vita kwa nguvu uvuvi haramu na kuhakikisha mazingira ya Ziwa yanakua mazuri ili samaki wazaliane kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.’’ Alisisitiza Dkt. Chilongani

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula alisema tayari kwa upande wa Wilaya ya Iramba Ziwa Kitangiri limeshafungwa toka tarehe 01 mwezi Januari na litafunguliwa tarehe 01 mwezi Aprili 2019

‘’ Ndugu Mkuu wa Wilaya ya Meatu kwa upande wetu tulikwisha funga Ziwa Kitangiri kama kawaida yetu ya kila mwaka isipokuwa mwaka huu tumeona tuje kujiriridhisha katika Wilaya ya Meatu maana miaka yote sisi tulikuwa tukifunga Ziwa upande wa Meatu wanavua hii ilikuwa inawatia unyonge sana wavuvi wa upande wa Iramba’’

Wakiwa katika  Kijiji cha Usulize Wilayani Meatu kwenye kambi ya wavuvi ya kijiji hicho Mheshimiwa mkuu wa Wilaya alitangaza rasmi  kufunga Ziwa hilo kwa uande wa Meatu.

‘’ Mkuu wa Wilaya ya Iramba na Wenyeviti wa Halmshauri zote na kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya hizi leo hii natamka kuwa Ziwa Kitangiri limefungwa hadi tarehe 01 mwezi Aprili mwaka huu hivyo kuanzia tarehe 17/04/2019 ndiyo Ziwa litafunguliwa Rasmi na shughuli za uvuvi zitaanza tena na yeyote atakayekiuka atachukuliwa hatua za kisheria’’ alionya Mkuu huyo wa Wilaya.

Kikao hicho cha ujirani mwema kimewaeleza wataalamu wa Halmashauri za Wilaya za Meatu, Iramba, Kishapu na Igunga ambao wananchi wake wanaonufaika na Ziwa hilo watengeneze Rasimu na kuweka sheria ndogo ndogo za kulinda Ziwa hilo na wamepewa mwezi mmoja kuandaa rasimu hiyo ambayo itakuwa ndiyo dira ya kudhibiti Ziwa hilo lisihujumiwe

MWISHO.

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.