• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

DC Meatu aongoza ziara ya Ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya lami.

Imewekwa: January 23rd, 2019

Na Linus R. James - MEATU DC

Mkuu wa wilaya ya Meatu Mh Dk. Joseph. E Chillongani mapema leo ameiongoza kamati ya Ulinzi na usalama ya wilaya ya Meatu, wakuu wa idara ya Halmashauri ya wilaya pamoja na taasisi  na viongozi wa siasa katika ukaguzi wa maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara mbali mbali za mitaa ya mji wa Mwanhuzi  za kiwango cha lami zenye jumla ya Kilometa moja na nusu.

Mradi huu ni kati ya ahadi alizozitoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 09 septemba 2018  katika viwanja vya Mwanhuzi wakati akiwahutubia wananchi alipotembelea Wilaya ya Meatu.

Kama ilivo ada ya kufanya vikao kabla ya kutembelea miradi mbali mbali Mkuu wa Wilaya alianza kikao hicho mapema asubuhi kwa kupokea taarifa fupi ya hali ya utekelezaji wa mradi kutoka kwa Meneja wa TARURA wilaya ya Meatu Mhandisi Mussa Miraji.

Meneja huyo alielezea kuwa mradi huu ni mkataba wa takribani  Tshs Bilioni 2.4 ambao unajumuisha Maswa na Meatu lakini meneja huyo alisema anatoa taarifa ya hali ya utekelezaji kwa upande wa Meatu pekee.

Mhandisi huyo alisema Mradi ulianza utekelezaji wake tarehe 26 Novemba mwaka 2018 ambapo utachukua jumla ya miezi mitatu kukamilika ivyo unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 24 Februari mwaka 2019.

Aidha alisema kuwa hali ya mradi ipo asilimia 60 na kazi zilizofanyika ni pamoja na kuweka vifusi na kuchimba mitaro ambapo kazi inaendelea.

Aidha alibainisha changamoto mbali mbali katika utekelezaji mradi ikiwa ni pamoja na mradi kuanza utekelezaji kipindi cha mvua, Wananchi kutokuheshimu alama za barabarani wakati wa ujenzi pamoja na mabomba kuwa ndani ya hifadhi ya barabara ambayo yamesababisha baadhi ya wananchi kukatiwa maji wakati wa utekelezaji wa mradi.

Pia Mhandisi huyo alikieleza kikao kuwa mradi huo licha ya kuwa unasimamiwa na TARURA wilaya, lakini kuna wasimamizi ngazi ya mkoa, na kitaifa ivyo aliwahakikishia kuwa barabara itakua ni ya hali ya ubora.

Baada ya kikao hicho Mkuu wa wilaya na timu yake walitembelea eneo lote la mradi na kujionea hali ya utekekelezaji ambapo alipata fursa ya kupata maelezo kutoka kwa Mkandarasi.

Akifanya majumuisho Mkuu wa Wilaya alisema kuwa hali ya mradi na ubora vinaridhisha.

“ Kuona ni kujifunza mengi Zaidi, lakini kuhusiana na ubora wenyewe , kwa jinsi wanavyomwaga vifusi  ukilinganisha na barabara iliyopo utaona kuna utofauti , Tulitaka kuona ubora, kasi ya kazi pamoja na changamoto za mradi”. Alisema Dk. Chillongani.

Mwisho kamati ilitoa maagizo kwa mkandarasi na Meneja wa maji kuhakikisha kuwa sehemu ambapo mabomba yamekatika yarudishiwe haraka ili wananchi waendelee kupata huduma ya maji.

Ivyo mkandarasi alimuomba meneja wa Idara ya Maji apeleke mapendekezo ya gharama za vifaa ili aweze kupatiwa fedha anununue vifaa na alete mafundi kwa ajili ya kuunganisha mabomba ifikapo kesho.

MWISHO.

Kupata picha zaidi bonyeza hapa

Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.