• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Meatu District Council
Meatu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Halmashauri ya Wilaya ya Meatu

  • Mwanzo
    • sub home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Miundombinu, Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Pre Primary Education
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango na Uratibu
      • Utumishi, Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha
      • Uratibu wa Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Expertise
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Fedha, Uongozi na Mipango
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha habari

Ajali yaacha simanzi kubwa Meatu

Imewekwa: June 10th, 2018

Na Linus R. James

Wananchi ya Wilaya ya Meatu wamekumbwa na simanzi kubwa leo kutokana na ajali iliyotokea mapema leo majira ya saa tatu asubuhi maeneo ya Kisesa kilometa chache kutoka Wilaya ya Itilima.

Ajali hiyo imetokea wakati msafara wa mwenyekiti wa UVCCM Taifa ndugu Kheri James ukitokea Itilima kuelekea Meatu kwa ajiri ya ziara mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukagua miradi na kusalimiana na wananchi pamoja na viongozi wa wilaya hiyo.

Akizungumza kwa njia ya simu Ndugu Hassan Hussein(Mabyelele) ambaye ni dereva wa Halmashauri ya Wilaya Meatu na ndiye alikua akiendesha gari lililowapakia waheshimiwa madiwani amesema gari la Halmashauri aina ya “Toyota Land Cruiser” lenye namba za usajiri STL 4981 limeharibika sana.

“Yaani ukiiona gari kwa nyuma haitamaniki, milango yote imevunjika, na ndo hiyo milango iliyombana Mheshimiwa mpaka akapata maumivu makali” Alisema Hassan

Baadhi ya Mashuuda mbali mbali waliokuwepo eneo la tukio wamesema chanzo cha ajali ni hitilafu iliyotokeaghafla (pancha)  katika mojawapo ya gari lililokuwa mbele ya msafara na ivo kupelekea baadhi ya magari yaliyokua yanalifuata kupunguza mwendo . Hata ivo wakati magari yanapunguza mwendo, basi lenye namba za usajili T617CXN mali ya ROMBO EXPRESS lilishindwa kusimama ghafla na ivyo kuligonga gari lenye namba STL 4981 kwa nyuma na kusababisha taharuki.

Katika harakati za uokoaji kulitokea ajali ya pili iliyohusisha gari la kiongozi lililokuwa kwenye harakazi za uokoaji wa majeruhi yaani kuwakimbiza majeruhi hospitalini kwa ajiri ya huduma ya awali, katika ajali hiyo gari hilo lilimkosa kosa Mtu mmoja na kisha kugonga mti maeneo ya Isengwa.

Katika ajali hiyo jumla ya watu 20 walipata majeraha mbalimbali na kukimbizwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Meatu na Kituo cha Afya Mwandoya na kupatiwa matibabu ya awali.

Aidha, Majeruhi mmoja alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Wilaya Meatu. Majeruhi aliyefariki anajulikana kwa jina la Mahega Masunga Selemani ambaye ni Diwani wa Kata ya Tindabuligi iliyopo Wilayani Meatu.

Majeruhi wengine kwenye ajali hiyo ni kama Mhe. Pius Z. Machungwa ambaye ni M/kiti wa Halmashauri Wengine ni Mhe. Juma I. Mpina, Mhe. Chalya Seni Igulu, Mhe. Daudi Matias Solo, Mhe. Seni Sita Mizumale, Mhe. Emmanuel Sayi Mboje, Mhe. Emmanuel Chalya, Mhe. Sasa G. Kishola, Mhe. Njile Ngwakwa, Mhe. Mlangale Sakumi, Mhe. Consolatha Lushu ambao wote ni Madiwani Kata mbali mbali Wilayani Meatu ambao baada ya kupata matibabu ya awali wamepata Rufaa Kwenda Hospitali ya Bugando Iliyopo koani Mwanza.

Wengine ni Ndg. Magreth Maneno, Ndg. Christina J. Hussein, Ndg. Daudi Masanja, Ndg. Bida Idaso, Ndg. Jeremiah Joseph, Ndg. Ngeleja Robert, Ndg. Philipo Malmala na Ndg.Christopher Mnanka ambao wengine wametibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani aidha wengine wapo wanaendelea na matibabu hospitali ya Wilaya ya Meatu

Ofis ya mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Meatu imeunda kamati kwa ajilia kutekeleza majukumu ya kuainisha mahitaji ya kufanikisha shughuli ya mazishi ya Mheshimiwa huyo pamoja na kuainisha gharama za kuwasaidia majeruhi waliopata rufaa. Jumla ya shilingi 5,872,500.00 zimetengwa ili kukamilisha maandalizi ya mazishi pamoja na kutoa msaada wa awali kwa Majeruhi waliapata rufaa.

Hata hivyo, mchanganuo wa fedha hizo ni kuwa kiasi cha shilingi 2,000,000.00 kitatumika kuwasaidia majeruhi na kiasi cha shilingi 3,872,500 ni kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya shughuli ya Mazishi.

Mazishi ya Mhe. Mahega Masunga Selemani yanatarajiwa kufanyika tarehe 13.06.2018 nyumbani kijijini Zebea kilichopo Wilaya ya Maswa.

Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Fabian Manoza anawapa pole ndugu, jamaa, marafiki wa wahanga wote waliokumbwa na tukio hili la kusikitisha. Aidha anawasihi wananchi wawe watulivu katika kipindi hiki kigumu na watumie mda huu kujumuika kumuombea marehemu na pia kuwaombea majeruhi wengine wapone haraka.



Matangazo

  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 16, 2024
  • Tangazo la Majina na Mipaka ya Vijiji na Vitongoji kwa Ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa September 16, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 20, 2024
  • Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Matokeo ya Mwanzo February 20, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi Karibuni

  • Jamii Yatakiwa Kupinga Mila Potofu, Kandamizi

    March 08, 2023
  • Meatu Pikipiki Tisa

    February 14, 2023
  • TAKUKURU RAFIKI

    January 27, 2023
  • Hongereni Wataalam: Ngatumbura

    January 27, 2023
  • Angalia zote

Video

Ziara ya Waheshimiwa mawaziri nane Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukusanya Maoni ya Kutatua Migogoro
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Miongozo Mbali mbali
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari
  • Dokumenti mbali mbali

Tovuti mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara ya Takwimu(NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Meatu, Simiyu, Tanzania

    Anwani ya Posta: S.L.P 44

    Simu: 028 2795 008

    Simu ya Mkononi: 0622 404 712

    Barua Pepe: ded@meatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meatu . Haki Zote Zimehifadhiwa.